Breaking News

TIB CORPORATE BENKI YATEKELEZA AGIZO LA RAIS MAGUFULI LA KUTOA HUDUMA SAA 24 BANDARI YA DAR

Benki ya Kibiashara ya Serikali ya TIB Corporate imenza kutoa huduma kwa masaa 24 za kukusanya kodi katika tawi Dogo la TPA kwenye Bandari ya Dar es salaam kutekeleza agizo la rais wa jamhuri wa muungano wa tanzania Dkt John Pombe Magufuli la kuzitaka taasisi zote zinazotoa huduma katika bandari ya Dar es salaam kuanza mara moja kutoa huduma zao kwa masaaa 24 hili kuongeza ufanisi.

Akizungumza leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo Bwana Frank Nyabundege alisema kufatia Benki hiyo kutiliana saini na Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) kwa ajili ya kuunganisha mfumo wa malipo ya kodi ujulikanao kama TAXBANK huduma ambao utafanyika bandarini hapo.

Alisema hatua hiyo itawezesha wananchi wote kulipia Kodi za aina mbalimbali pamoja na tozo za bandari kwani Benki hiyo imejipanga kuhakikisha inaleta ufanisi katika kutoa huduma.

Aidha Bwana Nyabundege aliongeza kuwa benki hiyo imejipanga kupanua wigo zaidi na kuboresha utoaji huduma za kibenki katika ukusanyaji wa  kodi hivi karibuni inatarajia kufungua matawi ya kutolea huduma katika Bandari ya Mtwara na Tanga pamoja na zingine ndani na nje ya Nchi.

Pia amevitaka vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa Wananchi kutambua kuwa kwasasa Benki hiyo imeanza kutoa huduma ya kulipia kodi katika Tawi Dogo la TPA lililopo ndani ya Bandari ya Dar es salaam kwa saa 24 kwa lengo la kuwarahisishia wanachi kulipa kodi zao bila usumbufu.