Breaking News

WASHINDI BETIKA "MTOKO WA KIBINGWA" KULA BATA LISILO NA MBAMBA

Dar es Salaam:
Kampuni ya michezo ya kubashiri Betika imesema msimu huu wa 5 imekuja kivingine na mtoko wa kibingwa kwa wateja wake watakao shinda kwa kutoa zawadi nono kwa dau la TSH 500 kupitia tovuti yao

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam katika halfa ya uzinduzi wa kampeni hiyo Meneja wa kampuni ya betika, Bwana Tumaini Maligana amesema MTOKO WA KIBINGWA BETIKA ni Kampeni inayosherekea Derby ya 3 kwa ukubwa barani Afrika Simba vs Yanga hivyo imekuwa ikiwaleta wateja wake kutoka Mikoa mbalimbali ikiwemo Kigoma, Sumbawanga, Kagera kutazama mechi uwanja wa Taifa na kuhudumiwa na ki VIP.

”Niwaombe watanzania kubeti kupitia tovuti yetu ya http://www.betika.co.tz ambayo menyu 14916# ili wasiwe watazamaji tu bali wawe miongoni mwa washindi 100″Amesema Meneja Maligana na kuongeza kuwa,

“Kuanzia msimu wa kwanza hadi wa nne Kampeni ya Mtoko wa kibingwa imekuwa na washindi 400 ambapo washindi wote waliletwa Dar es salaam kwa ndege kwenda na kurudi huku wakipatiwa simu za kisasa jezi hivyo Watanzania ni rahisi sana ubashiri wako uwe beti 5 yaani mikeka miatani yenye dau la TSH 500 na kuendelea kila mkeka usikose bahati yako “Alisema.

Alisema Mshiriki anayetaka kushinda anatakiwa kubashiri ligi mbalimbali ikiwemo EPL, LaLiga, Bundesliga na ligi za kibongo zikiwemo mechi ya Simba na Yanga.

Bwana Tumaini alibainisha kuwa zawadi Kwa msimu huu wa 5 Kampeni ya Mtoko wa Kibingwa utawawezesha washindi kuja Dar es salaam kwa usafiri wa ndege kwenda na kurudi kushuhudia mtanange kati ya watani wa jadi Simba na Yanga Aprili 16 Mwaka huu katika uwanja wa Be jamini Mkapa

“Tutakuwa na droo 10 za washindi kila wiki zitafanyika Moja kwa Moja kupitia vyombo vya habari nchini kote huku washindi wakitangazwa kila wiki hivyo hata washindi walioko Dar es salaam watapelekwa Uwanjani kwa msafara wa King’ola

Kwa upande wake Afisa Mahusiano na Umma wa Kampuni ya Betika bwana Juvenalius Rugambwa amesema kilele cha kampeni ya "haina Mbamba Kampeni ya Mtoko wa kibingwa" droo ya kwanza itafanyika Februari 13 mwaka huu ambapo washindi zaidi ya kumi watatangazwa kwani tunahitaji mabingwa 100 hivyo suka mikeka yako 5 kwa Tsh 500

“Hiii ni Derby Kubwa ya kihistoria na hao mabingwa tutawapatia malazi mazuri kwa kuwalaza hoteli ya nyota tano sisi Mtoko huu hauna Mbamba tumejipanga sana itakuwa siku ya kipekee kwa washindi kampeni hiyo inanza Leo na tutahitimisha Aprili 16 Mwaka huu.

No comments