TGNP Mtandao Yawajengea Uwezo Wanafunzi Wasichana Kutoka Vyuo Vikuu 10 Jijini Dar.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUds_8TRosRCxZVn0S0S21f2nCQi02GdYFyfhqs8t-cm3CLflOj1rh7sspndpGWJA4WGo-hPdXSZrQK0RU6A8A4aQOZAFeriVtGkbdhcPaeRPq5KxUzEl-K2vLAapZw_DOFKqYA1eCNZpH/s640/1.png)
Mkurugenzi wa TGNP Mtandao Bi. Liliani Liundi akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku nne kuwajengea uwezo wanafunzi wa kike juu ua ushiriki wamwanamke katika uongozi kutoka vyuo vikuu 10 jijini Dar es salaam.
TGNP Mtandao imeendesha
mafunzo ya uongozi maalumu kwa wanafunzi wasichana kutoka vyuo vya elimu ya juu
kwa lengo la kuwahamasisha na kuwajengea uwezo vijana wa kike kuwezesha kushiriki
katika kuwania nafasi za uongozi kuanzia ngazi ya vyuoni na nje ya vyuo.
Akizungumza wakati
wa ufunguzi wa mafunzo hayo jijini dar es salaam, mkurugenzi wa TGNP Mtandao
Bi. Liliani Liundi alisema mafunzo hayo ya sku nne yatajikita zaidi katika kuwanoa
na kuwapa ujasiri wa kuthubutu kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika
ngazi za maamuzi kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Alisema kwa mujibu
wa takwimu za Interpaliamentary Union (IPU) ya mwaka 2017 zinaonyesha kuwa ushiriki
wa wanawake katika uongozi katika ukanda wa afrika mashariki Tanzania imekuwa
mmoja ya nchi zinazofanya vizuri katika ushiriki wa wanawake katika nafasi
mbalimbali za uongozi.
“Tanzania ni moja
ya nchi zinayofanya vizuri katika ushiriki wa wanawake katika nafasi za uongozi
kwa kushika nafasi ya 2 kwa nchi za afrika ya mashariki na nafasi ya 25 duniani
kwa kuwa na asilimia 36 wa wabunge” Alisema Bi Liundi.
Bi liundi aliongeza
ikiwa bado atujafikia 50/50 pamoja na kwa mara ya kwanza tangu uhuru tumeweza
kuwa na mwanamke wa kwanza kuwa makamu wa rais Mama Samia Suluhu Hassan, Spika
wa Bunge la 10 Mhe Anna Makinda pamoja na Naibu spika katika bunge la 11 Mhe
Dkt Tulia Akson bado juhudi zaidi zinahitajika kuongeza nafasi za wanawake
katika ngazi za maamuzi.
Jumla ya wanafunzi
wa kike kutoka katika vyo vya elimu ya juu zaidi ya 10 kutoka dar es salaam, Arusha
na mkoani Morogoro wameshiki mafunzo hayo ya siku nne.
Baadhi ya washiriki
mafunzo ya siku nne kutoka katika vyuo
vya elimu ya juu zaidi ya 10 kutoka dar es salaam, Arusha na mkoani Morogoro jijini
dar es salaam
No comments