Waziri Kakunda: Hakuna Nchi Iliyoendelea Kufikia Viwanda Vikubwa Bila Kuhimiza Uendelezaji Viwanda Vidogodogo.
![Image result for waziri kakunda](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEik-fNCW5bjkLKf9OjOWnx_hd3aEkWiX1tVCXSY08Bcq9BwUVTdvkg-fkg-WjnOKlu5yEzMzdNKQKhavO_5dEYaV-dq69feQeY8PYpdslDEq2kkbLs_bD89OYXTmO5wpiLTMj8W9dG25W8/s640/1.jpg)
Waziri Kakunda amesema kuwa bila
kuhimiza uendelezaji viwanda vidogo vidogo ni vigumu nchi yeyote duniani
kufikia sekta yta viwanda vyenye tija kiuchumi kwa nchi.
“Hakuna nchi iliyofanikiwa
kiviwanda bila ya kuanza kusisitiza na kuhimiza kuviendeleza na
viwanda vidogodogo,SIDO ndio baba ya viwanda na mama viwanda hapa nchini kwa
hatua yake ya kuanza kumiliki viwanda vidogo”Amesema Waziri Kakunda.
Amebainisha kuwa Serikali ya
Awamu ya Tano inasapoti viwanda vidogovidogo lengo likiwa kufikia
uchumi wa kati kupitia sekta ya viwanda huku akisistiza,wananchi wakiendelea
kusapoti Sido itasababisha uchumi kukua.
Ameongeza kuwa viwanda vidovidogo
vikiendelea kuimarika vitapelekea kukuza uchumi wa n chi kwani bila sekta hii
nyingine haziwezi kupiga hatua kimaendeleo.
Katika hatua nyingine Waziri
Kakunda ameitaka Bodi hiyo kuhakikisha inaendelea na sekta ya
viwanda ikiwemo uongezaji ufanisi wa Sido taifa lipige.
Kwa Upande
wake Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la kuhudumia wenye viwanda
vidogo(SIDO),Profesa Elifas Bisanda amesema bodi hiyo itahakikisha wanaiweka
Sido kwenye ramani ya nzuri ili
kuvisaidia na kuviinua viwanda vidogodogo.
No comments