RUNGWE: UKAWA wanaitega NEC uchaguzi Siha, Kinondoni.
Hashim Rungwe
Mtego huo ni UKAWA kujiridhisha kama NEC inauwezo wa kuwadhibiti wakuu wa wilaya kutoingilia mchakato mzima wa uchaguzi.
Katika mahojiano maalum na matukio360, jijini Dar es salaam, mwenyekiti wa
chama cha Chauma, Hashim Rungwe amesema kilichofanywa na Chadema kinaungwa
mkono na Ukawa na kwamba walitangaza kurejea kwenye uchaguzi iwapo malalamiko
yao yatashughulikiwa na moja ya lalamiko lilikuwa ni wakuu wa wilaya
kuingilia uchaguzi.
"Hivyo katika hili NEC imetuhakikishia
kulishughulikia na tayari wamewaandikia barua viongozi hao wa wilaya kuwataka
kutojihusisha na uchaguzi Sasa tunataka kuona kama kweli wamerekebisha na
hatuwezi kuona kama tupo nje ya mpambano na kama hawajarekebisha tutazidi
kulalamika,” Alisema Rungwe
Rungwe amesisitiza walichofanya
Chadema ni maamuzi ya Ukawa kwa kuwa wakati wakiteua wawakilishi wa majimbo ya
Siha na Kinondoni vyama vingine vilikuwa na uwakilishi walioshiriki
kuwapitisha.
Walioteuliwa kugombea katika majimbo hayo ni Salum
Mwalimu Juma Kinondoni na Elvis Christopher Mosi jimbo la Siha.
Lakini kwa upande wake katibu mkuu wa NCCR-Mageuzi,
Danda Juju ameshangazwa na uamuzi huo na kwamba msimamo wa mwisho wa vyama
vinavyounda Ukawa ni kutoshiriki uchaguzi bado upo pale pale.
“Najisikia vibaya sana kuzungumza juu
ya suala hili, na kwa bahati mbaya waandishi wa habari wamekuwa wakiniulizia
kuhusu hili, nimekuwa sitaki kulizungumzia na pengine kwako wewe wacha nisema
hivi,”
“Labda kwa ufupi ni sema kwamba azimio
tulilokuwepo nalo la mwisho la vyama vinavyounda Ukawa bado liko palepale na
nilikuwa nazungumza na mwenyekiti wa kamati ya uongozi CUF juu ya hili, Chadema
wamefanya hivyo kama Chadema,” amesema Juju.
Amesema anatarajia kufanya mazungumzo
na Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif kujadili na kujua kilichojili na kwamba pia
watafanya juhudi za kukutana na Chadema ili kulijadili suala hilo kwa kina.
Juju amesema wakati Chadema
ikisimamisha wagombea bado yale waliyoyadai na shinikizo waliloweka NEC
hadi sasa matokeo yake hayajaonekana.
Amesema kuweka wagombea siyo vibaya
lakini ilitakiwa busara kutumika ili wakutane Ukawa kwa pamoja wazungumze ili
kuwa na mwelekeo wa pamoja
No comments