Naibu Meya Ilala Kumbilamoto Kukabidhi Mashine Ya Pamu.
Naibu meya wa Halmashauri
ya Manspaa ya ilala Omary Kumbilamoto anataraji kukabidhi msaada wa mashine ya kutibu
pumu katika zahanati ya vingunguti.
Akizungumza jijini dar
es salaam, Mhe kumbilamoto ambaye ni Diwani wa kata ya vingunguti alisema mashine
hiyo alinunua nchini dubai, baada ya kuona umuhimu wa uhitaji katika zahanati
yake.
“Wananchi wangu,
hasa wenye pumu ilikuwa inawalazimu kuchoma sindano, lakini mashine hii
itasaidia kutoa matibabu bila mgonjwa kuchomwa sindano” alisema Meya Kumbilamoto.
Alisema amepanga
kukabidhi mashine hiyo kwa uongozi wa zahanati hiyo ndani ya wiki hii.
Aidha Naibu meya
kumbilamoto aliongeza kuwa mashine hiyo ya kisasa yeye binafsi anaamini itasaidia
kwa kiasi kikubwa kupunguza athari za pumu kwa wananchi wake na kuhaidi
kuendelea kutatua changamoto zilizopo katika zahanati hiyo kwa kadri ya uwezo
wake ili wananchi wake wapate huduma bora za afya zinazo stahili.
Katika jitihada za
kuhakikisha anaboresha huduma mbalimbali kwa wananchi wa kata ya vingunguti hususani afya Naibu meya Omary Kumbillamoto
tayali ameshakabidhi gari ya kubebea wagonjwa ambalo ni tegemeo katika
halmashauri ya Manispaa Ya Ilala.
No comments