Breaking News

WAZIRI KAIRUKI: WATUMISHI HEWA NA VYETI FEKI BADO NI CHANGAMOTO

Image result for angela kairuki
Waziri nchi Ofisi ya Rais Menejimenti   ya utumishi wa Umma  na utawala bora  Mhe. Angela  Kairuki amesema Serikali bado inakabiliwa na changamoto kubwa ya watumishi wenye kughushi vyeti pamoja na watumishi hewa ambao walikuwa wakiendelea kupokea mshahara.
Akizungumza katika mkutano wa watumishi wa umma wa wilaya ya Kinondoni kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili alisema wapo baadhi ya watumishi waliokuwa wakilipwa mishahara ambao walishafariki na wengine tayali ni wastaafu pamoja na wasio na vyeti halali.
Alisema kwa kutambua hilo serikali ilianzisha zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumshi wa umma kote nchini zoezi ambalo limekuwa likifanyika kwa umakini mkubwa kupitia mfumo wa kanzidata kwa kushirikiana na RITA na TRA.
Aidha amewataka watumishi wa umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa mujibu wa sheria na kuzingatia maadili ya kazi hili kuongeza ufanisi zaidi.
Waziri Kairuki ametoa onyo kwa   watumishi wa umma wanaotumia vibaya nafasi zao kwa kuvujisha za taarifa ya serikali kuacha mara moja vinginevyo wakibainika hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Katika hatua nyingine waziri Kairuki Ametoa wito kwa watumishi wa umma kubadili mfumo wa maisha yao ili kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi na mengineyo yanayoambukiza sambamba na kufanya mazoezi ili kukabiliana na magonjwa yasiyoambukiza kama kisukari na presha.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Hapi amezitaja changamoto zinazoikabili wilaya ya Kinondoni kuwa ni upungufu wa watumishi katika idara ya Ardhi ambao wako nane tu hivyo amemuomba Waziri Kairuki kushughulikia suala hilo ili kurahisisha utendaji kazi katika wilaya hiyo sambamba na kusema kuwa jumla ya watumishi 144 wa sekta ya afya katika wilaya yake wamekutwa na vyeti feki.
Ziara hii ni mwendelezo wa ziara za Waziri Kairuki mkoani Dar es salaam kujadili changamotombalimbali zinazowakabili tayali amefanya ziara katika wilaya ya Temeke, Mbagala, Kigamboni na sasa Kinondoni ili kuzungumza na watumishi wa umma


No comments