CUF YA LIPUMBA YALAANI HUJUMA ZINAZOFANYWA NA CHADEMA KUPITIA MGOGORO WAO WA UONGOZI.
Chama cha wananchi (CUF)
kimelaani hujuma zinazofanywa kupitia matamko mbalimbali ambayo yamekuwa yakitolewa
na viongozi wa chama cha chama cha democrasia ba maendeleo (CHADEMA)
kuingilia mambo ya chama kwa kutumia mgogoro uongozi uliopo ndani ya chama
hicho.
Akizungumza Jijini Dar
es salaam Kaimu Katibu Mkuu Cuf Taifa Bi. Magdalena Sakaya alisema viongozi
wa chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kwa kushirikiana na Katibu mkuu
wa CUF Maalim Seif Sharrif Hamad wamekuwa wakitumia mgogoro uliopo ndani
ya chama hicho kwa lengo la kutaka kuifuta CUF upande wa Tanzania bara.
Alisema hujuma zinazopangwa
ni pamoja na kuvamia ofisi ya makao makuu ya chama hicho buguruni na sasa
wameenda mbali zaidi na kuamua kujitokeza kwenye kesi zilizofunguliwa na
washirika wao dhidi ya viongozi wa CUF kuwa nhujuma hizo azitafanikiwa kamwe.
Bi Sakaya amekitaka Chama hicho kujikita katika
kutafuta sababu za wanachama na viongozi wao kuhama katika chama chao na
kujiunga na chama cha CCM na si kuingilia kati mgogoro wa CUF ambao kimsingi
hauwahusu.
Aidha
aliongeza kuwa uwepo wa viongozi wa CHADEMA mahakamani katika kesi
zilizofunguliwa chama hicho ni ushahidi tosha wa maazimio ya vikao vyao vya
kutaka kukihujumu chama cha wananchi CUF na kuongeza kuwa chama hicho ndio wanahusika wakuu wa mgogoro unaoendelea ndani
ya CUF.
Mhe. Sakaya
amewakata wanachama wa CUF kuendelea kuwa watulivu kwani chama hicho kipo
katika mikono salama na kamwe njama zote zinazopangwa za kutaka kukihujumu chama
hicho azitafanikiwa kwani wao wanatekeleza na kukilinda chama kwa mujibu wa
katiba ya chama.
No comments