MHE KIGWANGALA: TUNAMBUA MCHANGO WA WADAU KATIKA KUBORESHA SEKTA YA AFYA
![Related image](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvqqkQKt8l0NueYjwfu2ncKfyvwYIxdkaSTDVeyLnGSwf4_JIK-2kAI6AXsOuXTmrXx_cw5Re6Pt08ZUgaPOPwCSA_ANuxrfAYa_IDwGMoO_n0eoS3sHX0nTCOLfunDdPYdw_PMPCYVgcz/s640/kigwangal3.jpg)
Serikali imesema
inatambua mchongo wa wadau na mashirika mbalimbali katika kusaidia kuboresha na
kupunguza changamoto zinayoikabili sekta ya afya nchini.
Akizungumza kwa Niaba
ya Waziri wa Afya, Mhe Dr. Hamis Kigwangala, Kaimu katibu mkuu wizara hiyo Bi.
Otilia Gowele aliesema serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuahikikisha upatikanaji
wa huduma bora za afya hususani kutoa elimu kwa wananchi juu ya afya ya uzazi.
Alisema serikali kwa kukishirikiana
na wadau wengine ikiwepo shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia idadi ya
watu duniani (UNFPA), kutoa elimu kwa wananchi kuhusu afya ya uzazi hili kukabiliana
na ongezeko la watu pasipo tija.
Aidha Bi. Gowele aliongeza kuwa
tafiti zinaonyesha kuwa katika kila dola moja ambayo serikali inawekeza katika
uzazi wa mpango mpaka dola sita zinaweza kuokoa shughuli nyingi za maendeleo
zikiwemo kupunguza umasikini, elimu na majanga mbalimbali yanayoweza
kujitokeza.
Kwa upande wake Mwakilishi mkazi
wa shirika la Umoja wa mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Dr.
Hashina Begum alisema uwekezaji wa uzazi wa mpango ni kuwekeza katika
afya pamoja na kuwekeza katika haki za wanawake duniani kote.
Alisema uzazi wa
mpango ukizingatiwa Taifa litakuwa katika nafasi nzuri katika kuendelea
uchumi na usawa wa kijinsia kufikia malengo 17 ya milenia ifikapo
mwaka 2030.
Maadhimisho ya siku ya kimataifa ya idadi ya watu duniani yanaadhimishwa
sambamba na mkutano wa kimataifa unaoendelea jijini London juu ya malengo
ya uzazi wa mpango kuelekea mwaka 2020, mwaka huu yamebeba kauli mbiu ya “Uzazi wa Mpango kuwezesha watu na
kuendeleza Mataifa”.
No comments