Breaking News

WAKAZI WA MANISPAA YA TEMEKE MWEMBE YANGA WAELEZEA ADHA YA DAMPO KARIBU NA MAKAZI



Wakazi wa manispaa ya  temeke mwembe yanga wamelalamikia kero kubwa wanazopata kutokana na dampo la uchafu ambalo limekuwa likisababisha kero kubwa kwao na kuwa tishio dhidi ya magonjwa ya milipuko ikiwemo kipindupindu.

Akizungumzia kero hiyo jijini Dar es salaam mkazi wa Temeke Shekh Jamal Twahir amesema kuwa tatizo hilo limekuwa sugu kwakuwa dampo hilo lipo maeneo ya makazi ya watu ambapo jumla ya kata kumi na nne zote zinaleta na kumwaga taka hapo katika kata ya Sandali na Tandika na kusema kuwa jambo linahatarisha afya za wakazi wa eneo hilo.

Kwa upande wake  mwinjilisti Cecil Simbaulanga ambae ni mkazi wa eneo hilo amesema kuwa wakazi wa eneo hilo wamekuwa wakipata shida kutokana na uchafu wa dampo hilo ambalo limekuwa linarundikana taka tofauti na wilaya nyinginezo.

Simbaulanga ameiomba serikali kuhamisha dampo hilo katika upande wa uwanja usiokuwa na makazi ya watu  ili wakazi wa eneo hilo wasiendelee kuathirika na taka hizo ambazo ni tishio kwa jamii.

Nae Juma Uweso amesema uwanja huu umekuwa ukitumika kwa shughuli mbalimbali za kitaifa, michezo lakini cha kushangaza ni kwamba uwanja huo huo umekuwa dampo lisilozolewa uchafu pindi shughuli za kitaifa zisipokuwepo.

Kero za dampo hilo zimekuwa changamoto kubwa kwa wakazi waishio kata ya sandari na tandika kwa kipindi kirefu sasa.

Sikilza mmoja ya wakazi wa emeo hilo akielezea==>>



No comments