Breaking News

SHEIKH PONDA: AMEITAKA SERIKALI PAMOJA NA BUNGE KUUNDA KIKOSI KUCHUNGUZA NA KUMALIZA MAUAJI YANAYOENDELEA MKOANI PWANI.

Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh  Ponda Issa

Dar es Salaam.
Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh  Ponda Issa ameitaka Serikali pamoja na Bunge kuunda kikosi cha watu kitakachoweza kusaidia kumaliza kabisa mauaji yanayoendelea kuripotiwa mkoani Pwani.

Akizungumza mara baada ya swala ya eid katika msikiti wa Magomeni kichangani alisema kitendo cha kuviachia Vyombo vya usalama peke yao bila ushirikiano na watu wengine hawawezi kumaliza tatizo hilo kwa haraka.

“Katika kipindi cha Ramadhani tumeshuhudia viongonzi wengine wanaendelea kuuwawa kiasi kwamba serikali inatakiwa kuongeza nguvu ya kutosha ilikutokomeza tatizo hilo” alisema Ponda

Alisema wabunge nao wanatakiwa kulitilia mkazo jambo hilo pamoja na kwenda kuongea na wananchi wa maeneo hayo na kuweza kujua chanzo cha tatizo juu ya mauaji hayo.

Sheikh  Ponda Aliongeza huenda wananchi wa maeneo hayo wanaogopa kuibua watu hao kutokana na njia inayotumiwa na Polisi ya kuwahoji wananchi hao na kuwakamata imekuwani ya kimabavu.

“Wananchi hao kwa sasa wameonekana wakiishi katika maisha ya hofu kiasi kwamba wanajamii wanatakiwa kuleta ushirikiano kwa jeshi la polisi ilikumaliza mauaji hayo.”alisema Ponda
 Sheikh Rajabu Katimba

Kwa upande wake Msemaji wa Taasisi hiyo, Sheikh Rajabu Katimba alisema kuwepo  kwa kikosi cha watu saidiaana na jeshi la polisi  kutaweza kusaidia kujua chimbuko la tatizo hilo.

Alisema wanaendelea kulaani vitendo hivyo vikundi hivyo vinavyo angamiza maisha ya wanadamu pasipo kujua wanahitaji vitu ganizaidi.

“Kibaya zaidi kinacho tusha ngaza zaidi kwanini mauaji hayo yanaangamiza watu wa jamii moja wizara husika inatakiwa kujua chanzo chake”. alisema Katimba

Aidha shekh katimba alishauri kuwa kama matukio hayo yanahushisha masuala ya kisiasa Serikali pamoja na bunge wanatakiwa kulitafutia ufumbuzi wa haraka.


No comments