MADEREVA DAR-BAGAMOYO WAMEIOMBA MANISPAA YA KINONDONI KUKARABATI KITUO CHA TEGETA NYUKI. DIWANI ATOA NENO…
Mwenyekiti wa Chama
cha Madereva Dar–Bagamoyo, Bw. Cliff Ngomuo, akifafanua kuhusu changamoto
mbalimbali wanazo kabiliana nazo katika kituo cha basi cha tegeta nyuki.
Dar es salaam:
Madereva wanaosafirisha
abiria kutoka stendi ya tegeta nyuki Dar kwenda Bagamoyo wameiomba manipsaa ya
kinondoni kukarabati miundombinu ya kituo hicho kwani imekuwa kero kubwa kutokana
na miundombinu yake kuwa katika hali mbaya.
Akizungunza na
waandishi wa habari kituoni hapo mwenyekiti wa chama cha madereva Dar–Bagamoyo,
Bw. Cliff Ngomuo alisema kufatia halmashauri kuwataka kuanza kutumia kituo
hicho badala ya makumbusho kero kubwa ni miundombinu ya kituo hicho hususani
barabara zinazoingia na kutoka kituoni hapo.
Alisema wao awana
tatizo na uhamuzi wa halmashauri ambao umewataka kuanza kuishia kituo cha tegeta
nyuki kama leseni zao zinavyoonyesha, bali mindombinu kituo hicho jambo ambalo
limekuwa kero kubwa kwao na watumiaji wa usafiri huo hususani usiku kutokana na
kutokuwepo taa.
Kamanda wa Polisi kikosi cha usalama barabarani wa wilaya ya
kinondoni,ACP Theopista Mallya akifafanua jambo mbele ya madereva na makonda
wanaosafirisha abiria kati ya Dar-Bagamoyo kuhusu leseni zao za kutoa huduma na
hatua ya kuwaondoa katika kituo cha makumbusho na kuishia tegeta nyuki.
ACP Theopista Mallya, alisema kwa mujibu wa leseni zao
wanatakiwa kuishia katika kituo hicho ila swala la wao kuwa wanaishia
makumbusho lilikuwa ni la mda tu hivyo kuwasisitiza kufata sheria na utaratibu
kama leseni zao zinavyowaelekeza.
“Kwa mujibu wa leseni zenu mnatakiwa kuishia tegeta
nyuki kwahiyo yeyote atakayekaidi agizo tayali atakuwa amevunja sheria sambamba
na kukiuka matakwa ya leseni zenu zinavyosema” Alisema.
Alisema pia ofisi yake tayali inaendelea
kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuchonga barabara za kuingia na kutoka
kituoni hapo kufatia mabasi kuanza kutumia kituo hicho alkini kutokana na mvua
zilizonyesha hivi karibuni zoezi hilo amelisitisha mpaka mvua zitakapoacha.
Bw. Urio aliongeza
kuwa pia ofisi yake imeshaleta wataalam hili kusanifu eneo hilo kuweza kuweka taa
kituoni hapo jambo ambalo limeshaanza kulitelekelezwa.
Mwonekeno wa kituo cha mabasi cha tegeta nyuki.
No comments