Breaking News

MEYA WA UBUNGO BONIFACE JACOB, ATOA UFAFANUZI JUU YA SAKATA LA KUMPATIA JINA LA MTAA VICTOR WANYAMA,AFUNGUKA HATA MBWANA SAMATA AKIJA UBUNGO TUTAMPATIA MTAA.

Asalaam ayelkum Watanzania,
Tangu jana kutoka habari ya kumpatia Jina la mtaa VICTOR WANYAMA, kata ya Ubungo na mtaa wa Ubungo N.H.C, nimeona kumekuwa na mijadala juu ya hilo, nimeamua nitoe somo juu ya jambo hilo kuepuka kuposhwa na wachambuzi uchwara.

Sheria namba 8 ya mwaka 1982 (sura namba 288) na sheria namba 6 ya mwaka 1999 ,ndiyo inayotoa mamla kwa serikali za mitaa kutunga na kutoa majina ya barabara za ndani ya halmashauri na barabara za mitaani.

*Soma sheria namba 8 ya mwaka 1982(sasa inaitwa sura 288) kifungu cha 55(1)j-to name or re name,where necessary,all streets(such names to be affixed in conspicuous places),and to cause the buildings in such streets to be numbered;*

TARATIBU ZA KUTOA MAJINA YA MTAA
Majina ya mtaa yana ngazi kuu tatu ya upatikanaji na upachikaji wa majina, katika mamlaka za serikali za mtaa, majina huanzia kwenye kamati za mtaa ndani ya serikali ya mtaa kwa mamlaka za miji na majiji kisha mapendekezo hayo huenda kamati ya mipango miji na mazingira ngazi ya wilaya na hutoka na azimio la kukubaliwa kwa jina pendekezwa.

Na baadae baraza la madiwani hupokea na kupitisha taarifa ya kamati ya mipango na mazingira.

NJIA ZA KUOENDEKEZA MAJINA YA MTAA
1. kwa viongozi wa kuu wa nchi kuleta mapendekezo ya kubadili au kutunga jina la barabara kama wana mgeni wa kitaifa.

2. Kwa mtu kujitolea kuwa mlezi wa barabara mtaani, ipitike vizuri basi huweza pewa jina lake.

3. kwa njia ya asili ya kufuatisha majina ya watu maarufu katika mtaa, mara nyingi hawa huwa hawaombi bali upendekezwa na wananchi.

4. kwa kikao cha kamati ya mtaa au wananchi kukaa na kupendekeza jina mara baada ya kuona wanasababu zao hapo mtaani kwao.

5. kwa kutoa kwa Heshima ya mgeni aliyetembelea mtaani kwao kama kumbukumbu ya mtaa husika na viongozi wake.

*SWALI*
*kwa nini Victor wanyama na siyo samata?*

*JIBU*
Mimi nilipokea ujumbe wa viongozi wa UBUNGO FOOTBALL ASSOCIATION (UFA) mapendekezo ya kuja mtaani kwangu kata ya ubungo siku ya jumamosi ya tarehe 24 June ya kwamba nitapokea ugeni wa wachezaji wa wili kuja mtaani kwetu, wageni waliotarajiwa kupokelewa ni Mbwana Samata wa Tanzania na Victor Wanyama (Kenya) kwa bahati mbaya alikuja mmoja ambaye ni Victor wanyama,ndiyo maana tukio linaonekana ni yeye tu amekabidhiwa jina la mtaa.

*SWALI*
Je Mbwana Samata akija ubungo mtampatia jina la mtaa*

*JIBU*
Tayari kamati ya mtaa ubungo N.H.C walisha kaa kikao na kukubali kuwapatia wachezaji hawa wa ulaya barabara mbili tofauti, ya Mbwana Samata zamani ilikuwa BENKI STREET (mita 800) na Victor Wanyama zamani iliitwa VIWANDANI STREET (mita 270) ambapo kwenye kikao chao cha mtaa mimi si mjumbe ila nilipendezwa na Idea ya mtaa wa N.H.C na kuwapa full support.

*SWALI*
*Kwa nini Victor Wanyama tu na siyo wanamichezo wengine maarufu wa zamani*

*JIBU*
Mimi ni kiongozi wa ngazi ya wilaya Ubungo na siyo kiongozi wa Kitaifa au Waziri wa michezo hivyo ninayo mamlaka ya kumsaidia mtu kupatiwa jina la mtaa katika ngazi yangu tu ili hao mnao wataja wapate mtaa huku halmashauri ya Ubungo tunawakaribisha waje wapokee barabara za kuzilea na kuzihudumia kama Victor Wanyama.

Pili, tulipendezwa na swala la victor kuja mtaani kwetu kutia hamasa vijana wetu wanaochezea ligi ya Ndondo cup, ligi yenye timu zisizo na madaraja rasmi TFF, hasa kipindi hiki cha mapumziko yake binafsi achilia mbali na utajiri wake, lakini akae kutimuliwa vumbi kiwanja cha kinesi, na kuwapa hali na mori vijana wa ubungo wenye ndoto kama yake ya kuchezea ligi za kulipwa ulaya.

Tunatamani wengine waje tuwape hadhi na heshima sawa na ya Victor Aliyo wapatia vijana wa ubungo, sembuse kuita jina la mtaa, tena wenye vumbi.

*Je na wewe unataka jina la mtaa wako?*
Ni rahisi sana chukua jukumu la kuhudumia moja ya barabara za mtaani kwako kisha nenda serikali ya mtaa unapoishi, waombe wakukabidhi rasmi barabara ya mtaa au fanya jambo lenye kuletea heshima na kuitangaza vema ndani na nje ya nchi halmashauri yetu ya Ubungo.

BONIFACE JACOB

MSTAHIKI MEYA UBUNGO
Senior Councilor*

No comments