Breaking News

RONALDO ATWAA TUZO YA BALLON D’OR. MCHEZAJI BORA WA DUNIA 2016,

Mshabuliaji wa Real Madrid amefunga mwaka kwa style ya pekee huku umri ukionekana kuelekea ukingo kwani mwaka huu amefunga magoli mawili ya Uefa Champions ila ndo mshindi wa Ballon d’Or.

Maana amefanikiwa kushinda tuzo ya mwanasoka bora wa dunia maarufu kama Ballon d’Or . Ronaldo sasa anaichukua mara ya nne, akiwa alianza mwaka 2008 akiwa Manchester United na alipoingia Madrid, unaweza kusema hii ni ‘hat trick’.
Kabla haijawa Ballon d’Or, Ronaldo alichukua mwaka 2008, Messi akachukua mwaka 2009.

Baada ya kuwa Ballon d’Or, Messi amechukua mara nne miaka ya 2011, 2012, 2013 na 2015. Huku Ronaldo akiwa amechukua mara tatu katika miaka ya 2013, 2014 na 2016.

Kumbuka alishinda Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Real Madrid, akashinda Kombe la Euro akiwa na Ureno.
Leo amebeba kura zaidi kati ya 173 zilizopigwa na waandishi duniani kote kwa usimamiza wa jarida maarufu la Ufaransa la France Football na kuwapiga bao Antoine Griezmann wa Atletico Madrid na Luis Suarez na Lionel Messi, wote wa Barcelona.


No comments