Breaking News

DKT. BITEKO AITAKA BODI YA TANESCO KUENDELEZA VYANZO VYA UMEME

Serikali imesema kuwa nishati ya umeme ni nguzo muhimu katika maendeleo ya kiuchumi ya Taifa na kuwa inachochea shughuli za uzalishaji viwandani, huduma na kuboresha maisha ya wananchi. Na ni matarajio ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuona umeme wa uhakika unafika kwa kila Mtanzania ili kuimarisha maendeleo na kuchochea kasi ya ukuaji wa uchumi.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko Septemba 15, 2024 jijini Dar es salaam wakati akizindua Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

No comments