Breaking News

Waziri Dkt. Mwigulu Azindua Tume ya Kutathimini Mapitio Na Maborsho ya Mifumo ya Ukusanyaji Mapato na Matumizi ya Serikali

Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba amezindua Tume ya Kufanya Tathimini  Mapitio na Maboresho ya Mifumo ya Ukusanyaji Mapato na Matumizi ya Serikali huku akibainisha uzoefu unaonesha nchi zilizoendelea zimepata mafanikio sababu ya kufanya mapitio na maboresho ya mifumo hiyo hivyo ni vyema nchi ikafanya hivyo.

Akizindua tume hiyo jijini Dar es Salaam Waziri Dk. Nchemba amesema nchi zilizoendelea zimefanikiwa kuwa na kiwango bora cha ukusanyaji mapato kutokana na kuwa mifumo thabiti na kwamba anaamini tume hiyo itatekeleza majukumu yake kikamilifu kwani ina wajumbe wenye uzoefu kwenye masuala ya fedha, mipango, mapato na matumizi.

"Tumeamua tupate wajumbe wa tume wa kuangalia mifumo ya mapato na matumizi watapitia mifumo na kufanya tathmini na maboresho itakayosaidia ongezeko la ukusanyaji mapato ya Serikali," amesema Waziri Dkt. Mwigulu.

Amebainisha kuwa tume hiyo itanza kufanya tathimini kwenye mifumo ya ukusanyaji mapato na kwamba itakapomaliza itahamia kwenye mngine ikiwemo tathmini ya ukuaji na ugharimiaji wa deni laSerikali, ulipaji wa mishahara, malimbikizo ya madeni  na ukuaji wake.

Amesisitiza kuwa uchumi wa nchi unakua kwa asilimia 6.4% hali iliyosababisha nchi kufikia hadhi ya uchumi wa kati kwani kiwango hicho cha uchumi kinatatarajiwa kiendane na ukusanyaji wa mapato.

Ameongeza kuwa wastani wa Nchi za Jumuiya ya Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC) ukusanyaji wa mapato huchangia asilimia 15.1% ya pato la taifa huku zilizoendelea hupata asilimia 40% ya pato hilo kuzifanya kuweza kugharamia miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Mjumbe wa Tume hiyo Profesa Nehemiah Usoro amesema watahakikisha wanatekeleza majukumu yao ili kufanikisha malengo yaliyowekwa katika kuboresha mifumo ya mapato na matumizi ya Serikali..

Tume hiyo inaundwa na wajumbe 10 ikiongozwa na Mwenyekiti wake Profesa Samweli Wangwe itafanya kazi kwa muda wa miezi sita kuanzia Agosti 25 mwaka huu.


No comments