Breaking News

TRL Yatangaza Ratiba Ya Treni Kwenda Bara Sasa Kuanzia Dodoma.

Kaimu Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji wa TRL Focus Sahani akizungumza na waandishi wa habari(hawapo pichani) makao makuu ya kampuni ya Reli (TRL) jijini Dar es Salaam.
*****
KAMPUNI ya relini nchini( TRL) imesema sasa safari  za treni zitaanzia Dodoma kwenda Kigoma , Mpanda na Mwanza.

Hatua hiyo imekuja kufuatia huduma za usafiri wa reli kutoka Dar es Salaam kwenda bara kusitishwa kutokana na mafuriko ya mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali  kuharibu miundombinu ya reli kati ya stesheni za Kilosa na Gulwe.


Hayo yemeelezwa na kaimu  naibu Mkurugenzi Mkuu wa Uendeshaji wa TRL, Bw.Focus Sahani akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya shirika hilo jijini dar es salaam kuhusu ratiba mpya ya huduma za treni kuanzia leo tarehe 16 Januari.

“Uongozi baada ya kufanya tathmini hali ya miundombinu ya maeneo mengine yaliosalama imeamua kuhamishia huduma ya usafiri wa treni kutokea Dodoma kuanzia Januari 16, 2018,” Alisema Bw. Sahani.

Akitaja ratiba hiyo, Sahani alisema treni ya abiria kutoka Dodoma itaondoka saa moja usiku siku ya Jumanne na Ijumaa kwenda Kigoma, Mwanza na Mpanda ambako inatarajiwa kuwasili Mwanza saa 12 jioni siku ya Jumatano na Mpanda saa 12 jioni na Kigoma saa 12:30 jioni.

Treni kutoka Mpanda, Mwanza na Kigoma zitatoka huko siku za Jumapili na Alhamisi tu. Mpanda itatoka saa 1:00 asubuhi, Mwanza itatoka saa 2:00 asubuhi na Kigoma itatoka saa 1:30 asubuhi. Treni hizo zinafika Dodoma siku ya saa 12:30 jioni.

Wakati huo huo alisema treni pekee ya kutoka Tabora kwenda Mpanda kurejea Tabora siku za Jumatatu, Jumatano na Jumamosi. Itakuwa inaondoka Tabora saa 12 asubuhi na kuwasili Mpanda saa 12:32 jioni. Itaondoka Mpanda kurejea Tabora saa 1:00 asubuhi na kuwasili saa 12:38 jioni.

Alisema mafundi wa kampuni hiyo wanafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kuwa kazi ya ukarabari na kurejesha katika hali yake maeneno yote inaendelea kwa kasi kati ya Kilosa na Gulwe hili kuweza kurejesha safari kama hilivyokuwa awali.

No comments