Breaking News

TGNP Yawanoa Wanawake Namna Ya Kuingiza Masuala Ya Jinsia Katika Biashara Wanaofanya Kazi Mipakani

Related image
Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) na Taasisi ya mafunzo ya jinsia (GTI) wameanza mafunzo ya siku tatu kwa ajili ya  kuangalia namna ya kuingiza masuala ya jinsia katika biashara kwa wanawake wafanyabiashara wa mipakani na wadau wake.
Akizungumza jijini DAR ES SALAAM, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP BI.LILIAN LIUNDI amesema kuwa mafunzo hayo yamewakutanisha washiriki 35 wakiwemo maofisa wa serikali kutoka mipaka tofauti, Asasi za kiraia pamoja na wafanyabiashara wanawake wanao jishughulisha na biashara mipakani.
Aidha amesema mafunzo hayo ni mwendelezo na yana lengo la kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kukabiliana na changamoto katika biashara sambamba na kuimarisha uwezo katika uingizaji wa masuala ya jinsia katika sera,mipango,bajeti miundo na michakato yote inayohusu biashara za mipakani.
Amebainisha kuwa utafiti uliofanywa na kituo cha sera za biashara Afrika (ATPC) umeonyesha biashara inatoa ajira kwa asilimia 60 ya wanawake katika biashara zinazofanyika katika nchi zilizopo  chini ya jangwa la sahara ambapo asilimia 70 na 80 ya wanawake hao wamejikita katika biashara isiyo rasmi. `
Kwa upande wake mshauri wa masuala ya jinsia na maendeleo BW.SULTAN MHINA amesema kuwa  zipo changamoto nyingi zinazoikabili nchi ya DEMOKRASIA YA CONGO hasa katika mahusiano ya kijinsia  kutokana na ukosefu wa uzingatiwaji wa sheria.

No comments