Breaking News

Shule Ya St Judith Yaibuka Mshindi Wa Kwanza Katika Shindano La Wanasayansi Chipukizi 2017.

Mwenyekiti wa Bodi Ya (YST) Profesa Yunus Mgaya Akiongea katika Hafla ya kukabidhi tuzo katika shindano la Wanasayansi Vijana (YST) jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Simoni Msangila Akiongea katika Halfa ya kuwatangaza washindi wa shindano la wanasayansi Vijana (YST) jijini Dar es salaam.

Wadau kutoka makampuni mbalimbali wakifatilia utoiaji wa tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika utafiti wa kisayansi (YST) mwaka 2017
Moja ya washindi wakikabidhiwa medani na kikombe katika mashindano ya wanasansi chipukizi (YST) ambayo yamekutanisha wanafunzi kutoka shule za sekondari nchi nzima bara na Zanzibar.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za sekondari nchini walioshiriki maonyesho ya ubunifu wa kazi za kisayansi kwa mwaka 2017 wakiimba wimbo wa taifa



Wadau kutoka makampuni mbalimbali wakifatilia utoiaji wa tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika utafiti wa kisayansi (YST) mwaka 2017.

Dar es salaam
Wanafunzi wa Shule ya Secondary ya St. Judith, Prosper Gasper na Erick Simon wametangazwa washindi wa kwanza katika mashindano ya ubunifu wa kazi za kisayansi 2017 yaliyowakutanisha wanafunzi kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na Zanzibar.

Wanafunzi hao ambao walibuni teknolojia ya kuzuia ajali ya moto kwa kutumia simu walijishindia Tsh 1.8 Milioni wanatajiwa kuwasilisha nchi nchini afrika kusini kushiriki mashindano ya wanasayansi chipukizi duniani ambapo yatafanyika mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa washindi wa shindano hilo mwanzilishi wa shindano la wanasayansi vijana nchini (YST), Dk Gozibeti Kamugisha alisema mashindano hayo yamejikita zaidi kuongeza na kutoa hamasa kwa wanafunzi hasa wa shule za secondary kupenda masomo ya sayansi.

Alisema kupitia shindano hilo ambalo linafanyika nchini kwa mara ya sita sasa limekuwa likiwakutanisha vijana kutoka sehemu mbalimbali nchini na kuwaleta pamoja ili waweze kuonyesha kazi zao za kibunifu ambazo walizoziandaa.

Dk. Kamugisha aliongeza kuwa kupitia kazi zao hizo za kibufu vijana hao wamekuwa wakipata wafadhili ambao wamekuwa wakiwasaidia kuendeleza mawazo yao hayo jambo ambalo limekuwa ni chachu kwa taifa kuweza kuwa na vijana walioiva katika maswala ya ki sayansi.

Alisema kupitia shindano hilo vijana wengi wameanza kuwa na mwako wa kupenda na kutamani kusomea masomo ya sayansi nchini ivyo kusaidia kuwezesha na `sera ya serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.

Mashindano hayo yamekutanisha zaidi ya wanafunzi mia kutoka shule za Secondary nchi nzima kushiriki kuonyesha kazi zao za kiugunduzi wa kisayansi ambapo mshindi wa kwanza ataungana na washindi wengine duniani katika fainali mashindano ya wanasayansi chipukizi yanayotaraji kufanyika nchini afrika ya kusini.

No comments