Breaking News

SAMSUNG YADHIDI KUJIDHATITI JUU YA KUPAMBANA NA BIDHAA FEKI.

Meneja bidhaa wa kampuni ya Samsung Tanzania Bw elias Mushi akizungumza katika mkutano waandishi wa habari makao makuu ua kampuni hiyo jijini dar es salaam.

Meneja wa Pyramid consumers ltd Bi kareen Babu akielezea walivyojipanga kufanya kazi pamoja na akiahidi wateja wasamsung kuwa watafanikisha kufikia soko la Tanzania kwa kiwango cha juu. 
Bi Lailatu Jethwa Retail manager SAMSUNG akitoa ufafanuzi juu ya stika hizo na serial namba ambazo zitatumika kama namba za usajili pindi unaponunua bidhaa zao ili uweze kushiriki katika droo hiyo. 
Meneja Uzalishaji wa kampuni ya Samsung Tanzania Bw Rayton Kwembe akifafanua juu ya stika hizo zitakavyowasaidia wateja wao kutambua bidhaa bora za kampuni hiyo.


Stika za kutambua ubora wa bidhaa za Samsung pamoja na wakala wa kuasambaza bidhaa zake

Dar es salaam
Kampuni ya vifaa vya teknolojia ya Samsung Tanzania imeanzisha mfumo mpya wa uwekaji stika mbili katika bidhaa zao kwajili ya utambuzi wa bidhaa halisi ikiwa ni njia ya kupambana na bidhaa feki hapa nchini.

Akitoa ufafanuzi mbele ya waandishi wa habari katika  makao makuu ya kampuni hiyo Jijini Dar es salaam, Meneja bidhaa wa kampuni hiyo Bw. Elias Mushi alisema stika hizo zitasaidia kutambulisha bidhaa halisi za kampuni hiyo ikiwa ni njia mojawapo ya kupambana na bidhaa feki.

Alisema bidhaa feki zimekuwa zikihatarisha maisha ya watumiaji hivyo matumizi ya stika hizo ni jitihada kampuni hiyo katika kukidhi matakwa ya wateja wa  Tanzania na ulimwenguni kwa ujumla.
Aidha Bw.Mushi alifafanua kuwa kuongezwa kwa alama  za stika hizo stika moja itakua ikionyesha jina la msambazaji na ya pili itakua stika inayotambulisha ubora wa bidhaa halisi ya Samsung.
Akizungumzia upatikanaji wa bidhaa zao bw Mushi alisema Samsung imeingia ubia na kampuni ya Pyramid Consumers ltd, kuwa ndio wasambazaji wao kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa bidhaa zao nchini nzima.

Kwa upande wake Meneja bidhaa wa Samsung Bi Lailatu Jethwa alisema kampuni ya Samsung Tanzania wamezindua kampeni ya “Nunua ,sajili, Na Ushinde “ itayoendeshwa kwa mwezi mmoja ikiwa ni kiunganishi cha kupeleka elimu kwa wateja wao na kupata uzoefu wa kuzitambua bidhaa halisi ya kampuni hiyo.

Alisema katika bahati nasibu hiyo ambayo kila siku atatangazwa mshindi 1 ambaye atajishindia bidhaa bora yenye waranti ya miezi 12 toka samsung kwa muda Wa mwezi mmoja.

Pia Bi Lailatu aliongeza kuwa hili kuweza kushiriki shinbano hilo unatakiwa kununua bidhaa yoyote ya Samsung kisha kujisajili kupitia namba za bidhaa (serial number) walizonunua kwa kutuma ujumbe mfupi (sms) kwenda 0798 222333.

Nae mkurugenzi wa kampuni ya Pyramid Consumers ltd, Bi Karem Babu-Selema alisema wateja wa bidhaa Samsung nchini watapata bidhaa bora kupitia kwa mawakala wao waliopo nchi nzima.

No comments