Breaking News

NAIBU MEYA ILALA, MHE OMARY NGUMILAMOTO KAMPUNI YA UJENZI YA DEL-MONTE KUONDOLEWA KATIKA LIST TENDA ZA UJENZI KATIKA MANISPAA HIYO.

Naibu meya wa Manispaa ya Ilala, Mhe Omary Ngumilamoto akisikiliza maelezo toka kwa kaimu Mhandisi wa manispaa ya ilala mhandisi Nyamagulula Masatu  katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya ujenzi iliyo chini ya manspaa hiyo
Naibu meya wa Manispaa ya Ilala, Mhe Omary Ngumilamoto akisikiliza maelezo kutoka kwa mkandarasi wa kampuni ya ujenzi ya Del Monte Bw Leornad Maguyani katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya manspaa hiyo.
Mkandarasi wa kampuni ya ujenzi ya Del monte Bw Leornad Maguyani akitoa maelezo juu ya mradi ujenzi wa barabara kutoka Mombasa hadi Mosha Baa kwa kiwango cha Lami yenye urefu wa kilomotea 1.65 ambayo itagarimu Bilioni Sh 2.4 katika ziara ya wajumbe wa kamati ya fedha ya manispaa ya ilala kukagua miradi inayoendeshwa na manispaa hiyoWajumbe wa kamati ya fedha ya manispaa ya ilala wakitembea kujionea ujenzi wa mradi wa barabra kutoka Mombasa hadi Mosha Baa katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya manspaa hiyo.

Na Frank Wandiba
Naibu meya wa Manispaa ya Ilala, Mhe Omary Ngumilamoto amesema wataiondoa Kampuni ya  ujenzi wa Barabara Del-Monte  katika tenda za ujenzi katika manispaa hiyo baada ya kujiridhisha kampuni hiyo imekuwa ikifanya kazi chini ya kiwango pamoja na kushindwa kumaliza kazi kwa wakati.

Kauli ya Mhe Ngumilamoto inakuja ikiwa ni tayali mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Mhe Paul Makonda  ambaye aliagiza viongozi wote wa manispaa za mkoa wa Dar es salaam  kutopia  tenda kampuni ya Del-Monte kutokana na kujenga barabara nyingi chini ya kiwango.

Alisema Kampuni hiyo ambayo imepewa tenda ya kujenga barabara kutoka Mombasa hadi Mosha Baa kwa kiwango cha Lami yenye urefu wa kilomotea 1.65 ambayo itagarimu Bilioni Sh 2.4  ujenzi huo umekuwa ukisuasua ambapo mpaka sasa kampuni hiyo tayali imeshalipwa milioni 301.

“Hii Kampuni ya Del-monte tulishakamtaa kutokana na miradi mingi tunayompa kushindwa kumaliza miradi kwa wakati  licha ya kupewa fedha lakini bado utendaji wake umekuwa usiolidhisha” alisema Ngumilamoto.

Ngumilamoto alisema Halmashauri hiyo tayali ilishaingia Mkataba na kampuni hiyo hivyo hawezi kumkatisha mkataba huo ila Mkataba wake utakoisha hawataendelea nayo sambamba na kuiondoa kampuni hiyo katika listi ya kampuni zinazopewa tenda na Halmashauri hiyo.

Aidha Mhe Ngumilamoto amemtaka Kaimu Mhandisi wa Manispaa hiyo, Bw Nyamagulula Masatu kuhakikisha anasimamia mradi huo unakamilika kwa wakati pamoja kuhusimamia ipasavyo kutokana na miradi mingi ya Barabara kujengwa chini ya kiwango hivyo kuharibika mda si mrefu tangu kukamilika kwa ujenzi wake.

Kwa Upande wake kaimu mhandisi wa Manispaa ya Ilala  Mhandisi Masatu alimhakikishia  Mhe, Ngumilamoto kuwa ataisimamia  mradi huo na kuhakikisha itaisha kwa wakati. 

No comments