Wajumbe Wa Bodi Mpya Ya TANROAD Wakagua Miradi Mbalimbali Inayoendelea Jijini Dar.
WAKALA wa Barabara
nchini (TANROADS) umesema kuwa miaka mitatu ijayo jiji la Dar es Salaam
litakuwa lenye kupendeza na kufanana kama ulaya baada ya miradi mikubwa mitano
inayoendelea kujengwa kukamilika.
Miradi hiyo
inayoendelea kujengwa jijini Dar es Salaam ni pamoja na Ubungo Interchange,
ujenzi wa jengo la tatu la abiria (Terminal III) katika kiwanja cha ndege cha
kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA TB III).
Mingine ni ujenzi
wa daraja jipya la Selander na barabara unganishi, upanuzi wa barabara ya
Morogoro kuanzia Kimara hadi Kibaha kuwa njia nane na Ujenzi wa Reli ya Kisasa
(SGR) kuanzia Dar es Salaam hadi Mwanza.
Akizungumza na
waandishi wa habari juzi baada ya ziara ya wajumbe wa bodi mpya ya TANROADS
kutembelea miradi inayosimamiwa na wakara huyo jijini Dar es Salaam, Mtendaji
Mkuu wa TANROADS Mhandisi Patrick Mfugale alisema jiji hilo litakuwa la tofauti
sana.
“Mi kazi yangu ni
kujenga ili jiji liiwe kama ulaya vile, si mmeona Aiport nani amesafiri nje ya
nchi, ile Terminal III inayojengwa imefanana na viwanja vingi duniani,” alisema
Mhandisi Mfugale.
“Miaka mitatu ijayo
maana yake 2022 litakuwa imebadilika sana, tutegemee foleni siyo nyingi,
tutegemee jiji litakuwa limependeza zaidi, mmeona wenyewe sasa hivi tunajenga
SGR juu kwa juu, reli kutoka bandarini tunategemea kwenda hadi Mwanza,”
aliongeza.
Akizungumzia mradi
huu, Mhandisi Mfagale alisema kuwa matarajio ni kwamba Desemba mwaka huu kwa
upande wa Morogoro Road utakuwa umekamilika.
“Tumeanza ujenzi
2017 na tutamaliza ujenzi kwa sehemu kubwa Desemba mwaka huu, niseme tu kwa
maka huu mwishoni Interchange kwa Morogoro Road itakuwa imekamilika, alisema
Mhandisi Mfugale.
Mhandisi huyo
alieleza kuwa kwa Interchange upande wa Barabara ya Mandela/Sam Nujoma
unatarajia kukamilika mwezi Mei mwakani 2019 na kusema kuwa kwa hatua ambayo
mradi huo umefikia haina shaka utakamilika kwa muda uliopangwa.
Alisema baada ya
kusaini mkataba mkataba wa Machi 22, 2017, Mkandarasi alianza kazi rasmi mwezi
Mei 2017. Kazi alizoanza nazo ni pamoja na matayarisho na kuhamisha miundombinu
ya maji, umeme, gesi na ya mawasiliano iliyokuwepo ndani ya eneo la ujenzi.
Alisema baada ya
kuhamisha miundombinu hiyo hatua iliyofikia ni kwamba ujenzi wa barabara za
pembeni imekamilika kwa asilimia 80 na magari yameshahamishiwa huko ili kupisha
ujenzi wa madaraja ya juu.
Kwa upande wake
Meneja Mradi huo kutoka TANROADS Mhandisi Barakael Mmali, alitaja kazi
zinazoendelea katika eneo hilo la ujenzi, baadhi ya kazi hizo ni pamoja na
upanuzi wa madaraja kwenye barabara za Nelson Mandela na Sam Nojuma ambao
umekamilika kwa asilimia 70.
Nyingine ni Ujenzi
wa barabara za pembeni kilometa 1.5 zilizokamilika kwa asilimia 80, ujenzi wa
misingi ya daraja (Piles) zenye kipenyo cha m.0.9m na urefu kati ya mita 22
ambapo nguzo 120 zimeshajengwa.
Mmali aliendelea
kubainisha kazi nyingine kuwa ni ujenzi wa vitako juu ya misingi ya daraja
ambapo vitajengwa jumla 39, hivyo kwamba maandalizi ya ujenzi wa vitako vitano
unaendelea na ujenzi wa nguzo za daraja kutoka kwenye vitako kwenda juu ya
ardhi ambapo jumala ni 64 hivyo maandalizi yanaendelea.
Mhandisi Mmali
alisema hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umedikia asilimia 25 na umepangwa
kukamilika mwishoni mwa Desemba 2020.
Mradi huu wenye
thamani jumla ya sh.bilioni 247 kati ya fedha hizo sh.bilioni 200 ni mkopo
kutoka Benki ya Dunia ndani ya mradi wa mkuu wa kuboresha usafiri jijini
Dar es Salaam uitwao “Dar es Salaam Urban Transport Improvement project” huku
serikali ya Tanzania ikichangia sh.bilioni 47.
Daraja la Selander
Alisema ujenzi wa
daraja hilo unaendelea vizuri na kueleza kuwa hatua iliyofikia sasa ni ujenzi
wa daraja la muda ambalo limefikia urefu wakilometa 1.05.
Alisema daraja hilo
litatumika kusafirishia vifaa wakati wa ujenzi wa daraja lenyewe.
“Na mmeona progress
kwa sasa ni asilimi 5.3 na tulitegemea iwe 5.2 kwa hiyo mkandarasi yupo sawa ,
kwa hiyo atamaliza kazi kwa muda uliopangwa, tumeangalia na mmeona jinsi zile
nguzo anavyoziingiza na mashine zake zote zimeshafika kwa hiyo hatuna wasi wasi
nae,” alisema Mhandisi huyo.
Daraja hilo lenye
urefu wa meta 1,030 na upana wa meta 20.5 litakuwa na njia 4 za magari na
njia 2 za watembea kwa miguu, na litajengwa pamoja na barabara unganishi zenye
jumla ya kilometa 5.2
Mradi huu
utagharimu shilingi Bilioni 256 zilizotolewa kwa mkopo nafuu kutoka Jamhuri ya
Korea kupitia Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi (EDCF) na Serikali
ya Tanzania.
Daraja hilo
lintarajia kudumu kwa muda wa miaka 100 na litajengwa bila kuathiri nyumba
zilizopo kando ya barabara za Kenyatta na Toure ambazo miongoni mwake wanaishi
Mabalozi.
Mhandisi Mfugale
alisema kuwa TANROADS pia imepewa kujeinga mradi wa viwanja vya ndege ambapo
kwa sasa wanasimamia ujenzi wa ujenzi wa jengo la Terminal III.
Alisema tangu 2013
lilikuwa linajengwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) lakini TAA 2017
waliwakabidhi kuujenga mradi huo.
Alsema hadi sasa
mradi umekamilika kwa zaidi ya asilimia 90 na kwa mujibu wa mkataba mradi
utakamilika Mei 31, 2019 kwani kila kitu ni kama kimekamilika kazi iliyopo ni
kumalizia kupaka rangi na kufanya usafi wa jengo.
Aliongeza kuwa
jengo hilo litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kubeba abiria milioni 6 kwa
mwaka tofauti na Terminal II ya sasa inayochukua abiria milion 2 kwa mwaka.
Barabara 8 Kimara
hadi Kibaha
Alisema mradi huu
ulipangwa kufanyika kwa miezi 30 kuanzia Julai 21,2018 ambapo unagharimu kiasi
cha shilingi Bilioni 141.56 Fedha zote kutoka serikali ya Tanzania na
unasimamiwa kwa asilimia na TANROADS wenyewe.
Mradi huo Utakuwa
na umbali wa kilomita 19.2 na utahusisha upanuzi wa njia nane, njia mpya kabisa
sita zitajengwa, tatu kwenda Dar es Salaam na tatu kwenda Morogoro na mbili
zilizokuwepo.
“Lakini za zamani
zile za katika kati tutaziboresha zaidi ili ziungane na hizo barabara mpya
zinazojengwa,” alisema Mhandisi Mfugale.
Mradi huo muhimu
ukikamilika utasaidia kupunguza msongamano mkubwa wa Magari takribani 50,000
yanayopita katika barabara hiyo kila siku .
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa bodi Dk. Dalmas Nyaoro alikiri kuridhishwa na miradi hiyo
inavyoendelea, lakini aliishauri TANROADS kuwa karibu na wakandarasi ili
kuwasimamia na kuhakikisha wanajenga miradi hiyo kwa ufanisi.
“Ushauri wetu kwa
tanroad ni vizuri wakawepo wakati wakandarasi wanajenga ili kujiridhisha kwamba
hiki walichosema watajenga ndiyo hicho wanchojenga,” alisema Dk. Nyaoro.
Alieleza kuwa kama
hawatakuwepo tatizo katika mradi likitokea hawawezi kujua kama tatizo lilikuwa
ni usanifu ama ni mkandarasi.
“Ni kwamba
TANROADS wawe na mtu wao kwenye eneo la mradi ambaye anasimamia kwa
karibu na kuhakikisha kwamba kile kinachotakiwa ndicho kinachofanyika,”
aliongeza.
Alisisitiza
“Wanatakiwa kuwa makini hususani upande wa ujenzi wa msingi kwani ukishaweka
kitu chini ya ardhi huwezi ukajua chini kuna nini kama hukuwepo, huku juu
unaweza ukajua, lakini chini ya ardhi ni vizuri kujihakikishia wakati
wanajenga,”.
Aidha alipongeza
ujenzi wa mradi wa barabara za juu unaoendelea eneo la Ubungo kwa kusema kuwa
kazi inakwenda vizuri na kueleza kuwa ukikamilika utamaliza tatizp la foleni.
No comments