Breaking News

Mhe Said Soud Said Mwenyekiti Taifa Chama Cha AFP

Mwenyekiti Wa Chama Cha Wakulima Taifa (AFP) Mhe. Said akimzungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu Taifa mara baada ya kutangazwa mshindi wa kishido kwa kupata kura 97 kati ya 102 jijini Dar es salaam.

Dar es salaam:
Wajumbe Wa Mkutano Mkuu Taifa Wa Chama Cha Wakulima Tanzania (AFP) Wamemchagua Mhe. Said Soud Said Kuongoza Tena Chama Hicho Kwa Kipindi Cha Miaka Nne Baada Ya Kupata Kura 97 Kati Ya Kura 102 Za Wajumbe Wote Wa Mkutano Mkuu Wa Taifa.

Mhe Said Ambaye Alikuwa Anatetea Nafasi Hiyo Katika Uchaguzi Huo Alikuwa Mgombea Pekee Wa Nafasi Ya Mwenyekiti Taifa Alipata Kura Za Ndio 97, Kura 3 Za Hapana, Wajumbe 2 Hawakupiga Kura.

Pia Wajumbe Wa Mkutano Huo Wamemchagua Bw. Kilindo Saidi Kuwa Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara, Na Mhe. Juma Saidi Amary Kuwa Makamu Mwenyekiti Uoande Wa Zanzibar.

Akizungumza Mara Baada Ya Kutangazwa Mshindi Mwenyekiti Wa Chama Cha Wakulima Taifa (AFP) Mhe.Said Soud Said Aliwashukuru Wajumbe Wa Mkutano Mkuu Wa Taifa Kwa Kuwa Na Imani Nae Na Kumpa Kura Za Ndio Za Kutosha.

Alisema Ataendelea Kudumisha Umoja Na Mshikamano Uliopo Ndani Ya Chama Hicho Hili Kuweza Kufikia Malengo Ya Kikatiba Ya Kuanzishwa Kwa Chama Hicho Hili Kiweze Kushika Dola.

Alisema Umoja Na Mshikamano Ndio Silaha Pekee Kwao Kuweza Kufikia Malengo Waliojiwekea Kama Chama Sambamba Na Kutekeleza Sera Za Chama Hicho Ambacho Kwa Asilimia Kubwa Wanachama Wake Ni Wakulima.

Mkutano Huo Umewapitisha Mhe. Rashid Rai Kuendelealea Kuwa Katibu Mkuu Taifa Kwa Kipindi Kingine Cha Maiaka Nne, Sambamba Na Abdul Ngakolwa Naibu Katibu Mkuu Bara Na Mhe Salum Masuud Naibu Katibu Mkuu Zanzibar.

Pia Wajumbe Wa Mkutano Huo Pia Wamewachagua Bw. Isidory Mhemela Kuwa Mwenyekiti Wa Vijana Taifa Sambamba Na Bi Rehema Nassoro Ligawandu Kuwa Katibu Wa Vijana Taifa.

Jumla Ya Wajumbe 102 Kutoka Tanzania Bara Na Zanzibar Wameudhulia Mkutano Huo Ambao Umefanyika Jijini Dar Es Salaam


Wajumbe Wa Mkutano Mkuu Wa Chama Cha Wakulima Tananzania (AFP) Wakifatilia Mada Mbalimbali Katika Mkutano Huo Uliofanyika 10 Feb 2018 Jijini Dar Es Salaam
Mwenyekiti Wa Mkoa Wa Lindi Mhe. Abdull Azizi, Kushoto Akiwa Na Msajili Msaidizi wa Vyama Vya Siasa Bw. Siyst Leonard Nyahoza Nje Ya Ukumbi Ulikofanyika Mkutano Mkuu Wa Taifa Chama Cha Wakuliama Tanzania (AFP) Jijini Dar es salaam.

No comments