Breaking News

Dc Mjema Ahaidi Kujenga Visima Viwili Kumaliza Tatizo Sugu La Maji Wakazi Wa Kata Ya Kiwalani.

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe.Sophia Mjema ameaidi kuwajengea visima viwili wakazi wa Kata ya Kiwalani ambavyo vitasaidia kuondokana na tatizo sugu la maji linalowakabili.

Akizungumza na wananchi katika mkutano wa wananchi na viongozi wa kata hiyo uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Yombo Kiwalani mara baada ya kushiriki zoezi la kufanya usafi katika Chuo cha ufundi cha  watu wenye Ulemavu.

Alisema maisha ya kila siku ya mwanadamu anategemea maji katika kuendesha shughuli zake mbalimbali hivyo atahakikisha anashirikiana na viongozi na wananchi wa kata hiyo kuhakikisha wanamaliza changamoto ya upatikanaji wa maji katika kata hiyo.
Alisema wakati  wananchi wa kata hiyo wakisubiri mradi mpya wa Shirika la Majisafi na Majitaka (Dawasco) ili iwatatulie tatizo la  maji hivyo amewahakikishia atawajengea visima viwili vya maji baada ya utaratibu kukamilka.

“Katika suala la maji nitahakikisha wana wananchi mnapata maji safi na salama nyinyi na viongozi wenu mtapanga kupanga maeneo ya kujenga “ Alisema Mhe Mjema.
Aidha akizungumzia kero ya usalama katika kata hiyo kufatia kutokuwepo na kituo cha polisi amewataka viongozi  wa kata kuandaa eneo maalumu kwa ajili ya kujenga kituo cha Polisi yeye kama mwenyekiti wa kamati ya ulizi na usalama atahakikisha anasimamia ujenzi wa kituo hicho hili kuwasaidia wananchi kupata huduma wakati wowote.
“Vijana wengi wapo mitaani hawafanyi kazi yeyote wanashinda usiku kucha katika mabar na vijiwe jambo ambalo linapelekea vijana haonkujiingiza katika wimbi la kufanya vitendo vya uharifu” Alisema Mhe. Mjema
Pia Mhe Mjema amewataka wamiliki wa viwanda kuhakikisha wanaajiri wazawa ili kuepusha migogoro inayoendelea kwani kwa kufanya hiyo kutasaidia kupunguza tatizo kubwa la ajila kwa vijana pamoja na kupumguza wimbi kubwa la Vijana wanaokaa mitaani mpaka usiku wamanane bila shughili maalum hivyo kuwa ndio chanzo kikubwa cha vijana wengi kujigiza katika matukio ya uporaji.
Alisema kuna kazi nyingi za kufanya hasa kwa vijana wazawa kama usafi na ulinzi hivyo wamiliki wa viwanda wanatakiwa kuwaajiri wasiegemee kuwaajiri watu kutoka nje ya nchi.
Kwa upande wake MKuregenzi wa Manispaa hiyo, Bw. Msongela Palela aliwataka viongozi wa Serikali za mitaa kujiepusha vitendo vya rushwa pindi wananchi wanapohitaji huduma kama kusainiwa barua zao za kujiunga na vikundi mbalimbali.

“Ukiona kiongozi yeyote wa serikali anapokea hela kwa ajili ya kugonga muhuri usisite kuniletea taarifa ofisini kwangu ili niweze kumchukulia hatua za kisheria” Aalisema Bw. Palela.

No comments