Breaking News

Ziara Ya Mbunge Wa Temeke Mhe Abdallah Mtolea Kutembelea vikundi vya wajasiliamali jimboni kwake.

Mbunge wa Temeke Mhe. Abdallah Mtolea akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika ziara kutembelea vikundi mbalimbali vya wajasilimali jimboni kwake.

Mhe.Mtolea akifafanua jambo kwa Bi Magg Mum kutoka taasisi ya Global Fondation ya nchini uingereza katika ziara ya kutembelea vikundi mbalimbali vya ujasiliamali jimboni kwake.



Mbunge wa temeke Mhe. Abdallah Mtolea, pembeni yake ni Bi Magg Mum akisikiliza maelezo global Foundation ya nchini uingereza kutoka kwa moja ya wasimamizi wa studio ya kurekodia maigizo (sinema) na mziki wa kizazi kipya katika ziara hiyo.

Dar es salaam
Mbunge wa jimbo la temeke Mhe. Abdallah Mtolea amefanya ziara ya kutembelea vikundi vya wajasiliamali kukagua na kuona changamto wanazokutana nazo wakati wa kutekeleza majukumu yao.

Akizungumza katika ziara hiyo jijini Dar es salaam Mhe. Mtolea alisema  lengo la ziara yake ni kujionea namna wajasiliamali hao wanavyofanya shughuli zao pamoja na kusikiliza changamoto zao hili aweze kuzitafutia ufumbuzi.

Alisema kwa kutambua ukosefu wa mitaji pamoja na mazingira ya kufanyia kazi zao sambamba na teknolojia duni ni moja ya vikwazo wanavyokutana navyo wajasiliamali hata mara baada ya kuwezeshwa.

Amezitaja changamoto nyngine ni upatikanaji wa masoko ya  uhakika wa bidhaa wanazozizalisha pamoja na kutokuwepo na maeneo rasmi ya kufanyia biashara zao.

Akizungumza mara baada ya kuwasili Mhe mtolea katika kikundi chao msimamizi wa kituo cha Temeke Youth Hope saccos (Mwela Theater Group) Bw.Hamadi Jongo aliesema anamshukuru Mhe mbunge kwa kuwawezesha kikundi hicho kinachojishughulisha na kuuza mayai na kuku kuwa mkombozi kwa vijana.

Alisema kupitia kikundi hicho vijana wameweza kujikwamua kiuchumi sambamba na kuwawezesha kuweza kufikia malengo yao kama vijana.

Nao kikundi cha  kinamama cha Tupambane na Umaskini Tuendelee ambacho kilianzishwa kwa kushirikiana na ofisi ya mbunge kimekuwa na mafanikio tangu kuanzishwa kwake 2016 kufatia kupatiwa mafunzo namna bora ya kujiendelesha yaliyotolewa na kampuni ya Naimango Business Agency ya jijini Dar es salaam.

Walisema kikundi hicho kinaendesha mradi wa kufuga kuku wa kisasa ambao walianza na kuku 158 na kwa sasa wana jumla ya kuku 950.

Aidha Wamemwomba mhe mbunge kuwasaidia kupata eneo waweze kukuza mradi wao kuku hili kujenga banda kubwa zaidi, kuanzisha mradi wa kufuga samaki  wa biashara pamoja na kulimba mboga mboga na matunda.

No comments