Breaking News

Mhe Samia Kuzindua kongamano la wanawake tarehe 26 mwezi huu Jijini Dar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania he Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la uhamasishaji na uwezeshaji kiuchumi mkoa wa dar es salaam utakaofanyika tarehe 26 mwezi huu.

Akizungumza na waandishi mapema leo jijini dar es salaam Mkuu wa wilaya ya ilala Mhe Sophia Mjema alisema uzinduzi huo ambao utawakutanisha wanawake zaidi ya 3000 kutoka katika manispaa zote tano za jiji umelenga kuwakutanisha kushauliana namna ya kutatua changamoto zinazowakabili na kuzipatia ufumbuzi.

Alisema jukwaa hilo litatoa fursa kwa wanawake kutoka katika Nyanja mbalimbali za uzalishaji kukaa pamoja na kubadilishana mawazo pamoja na kupewa mafunzo juu ya njia bora za kuboresha biashara zao hili kujikwamua kiuchumi.

“kupitia jukwaa hili wanawake kutoka manispaa zote za jiji la dar es salaam watakutana na kukaa pamoja kubadilishana uzoefu na kupatiwa mafunzo namna wanavyoweza kutatua changamoto wanazokutana nazo pamoja na kupatiwa ushauri wa kitaalam namna ya kuendesha shughuli zao” Alisema Mhe Mjema.
Kwa upande wake katibu mtendaji wa baraza la uwezeshaji (NEEC) Bi Beng’I Issa amewataka vijana na wanawake kujitokeza kwa wingi siku hiyo hili kuweza kupatiwa elimu juu ya kurasimisha biashara zao.

Alisema taasisi mbalimbali zitashiriki Shirika la viwanda vidogo vidogo (SIDO), Shirika la viwango Tanzania (TBS) na Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA), watatoa mafunzo na kutoa vibali kwa wakina mama wanaendesha shughuli za uzalishaji pamoja na kuwapatia vyeti baada ya kupatiwa mafunzo ya kuboresha bidhaa zao.

No comments