Breaking News

Meya Mwita Aishukia Nssf Malipo Bilioni 40 Ya Ujenzi Wa Machinga Complex

Meya wa Jiji Mhe Isaya Mwita
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam limemuomba waziri  nchi ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa, Mhe George Simbachawene pamoja na waziri wa fedha na mipango Dkt. Philip Mpango kuangalia namna ya kutatua mgogoro uliopo kati halmashauri ya ya Jiji na mfuko wa hifadhi ya jamii wa (NSSF)  katika jengo la Dar es Salaam City Council Business Park maarufu kama (Machinga Complex) kuafatia halmashauri ya jiji kutakiwa kulipa deni la zaidi ya Bilioni 40  kinyume na mkataba.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mapema leo Meya wa Jiji, Mhe Isaya Mwita alisema amefikia hatua ya kumtaka Waziri Simbachawene kuingilia kazi mgogoro huo kutokana na kutorizika na hatua ya NSSF kuwataka walipe bilioni 40 tofauti na mkataba  unavyotaka walipe bilioni 12.45 .

Alisema halmashauri ya jiji la Dar es Salaam ilingia mkataba  wa ujenzi wa jingo hilo na NSSF  kwa mkopo wa shilingi bilioni 10 na mkataba huo ulifanyiwa mapitio ambapo mkopo huo gharama ziliongezeka na kufanya mkopo kufikia shilingi bilioni 12.45.

''Lakini makabidhiano  ya jengo yalifanyika mwaka 2010 garama jengo ilikuwa ni Bilioni  12.7 kwa  sasa  tunashangaa tunaambiwa na hawa watu kuwaeti deni hilo linaladaliwa kuwa zaidi ya bilioni 40 sio bilioni 12.7 hatuwezi kukubali kabisa " Alisema Mhe Mwita.


Aidha Mhe Mwita aliongeza kuwa Halmashauri ya jiji imebaini kuwepo na ukiukwaji mkubwa wa kimkataba katika hatua za ujenzi wa jengo hilo kwakuwa mkataba unalitaka jengo hilo liwe na vizimba elfu kumi lakini badala yake limekuwa na vizimba elfu nne tu  pamoja na gorofa  ilitakiwa kuwa na gorofa tano upande mmoja na ghorofa  sita upande mwingine  lakini  wamepewa jengo lenye gorofa nne kinyume na mkataba .

Alisema tangu alipoingia madarakani uingoza Halmashauri ya jiji amekuwa akifanya jitihada za makusudi kwa muda mrefu kutafuta muafaka  na NSSF juu ya ulipaji deni hilo bila mafanikio.

"Kwa kutambua  umuhimu wa urejeshaji wa fedha hizo ambazo zinazotokana  na michango ya wanachama wa mfuko huo na kwa kuzigatia  hali halmahsauri ya jiji tumebaini deni hilo halilipiki'' Alisema Mhe Mwita.

Pia Mhe Mwita aliongeza kuwa jiji wako tayari kulikabidhi jengo hilo kwa NSSF ili wao waliendeshe  ili waweze kurejesha  fedha  zilizotolewa na mfuko huo kama mkopo kwa halmashauri ya jiji  kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo kutokana na jiji hilo kushindwa kulipa deni hilo.


Alisema Mkataba ulitaka  NSSF  kutoa fedha  kwa Halmashauri  ya Jiji kwa ajili ya ujenzi  wa jengo hilo jambo ambalo halikufanyika hivyo Halmashauri hiyo haikuhusika na usimamizi wa fedha zilizokopwa  na kuifanya  kushindwa  kuthibitisha gharama  zilizotumika .

No comments