PROF LIPUMBA AWAVUA UANACHAMA WABUNGE NANE WA VITI MAALUM PAMOJA NA MADIWANI WAWILI KWA KOSA LA KUKISALITI CHAMA
Baraza
Kuu la Uongozi CUF chini ya mwenyekiti anaetambuliwa na msajili wa vyama vya
siasa nchini Prof Ibrahim Lipumba leo limewavua uanachama Wabunge Nane wa Viti
Maalum pamoja na Madiwani Wawili kwa kosa la kukisaliti chama.
Akizungumza makao makuu ya chama buguruni jijini Dar es
Salaam Mwenyekiti wa chama Prof Ibrahim Lipumba alisema wabunge
hao na madiwani waliitwa katika kamati ya nidhamu ya chama Jana kuhojiwa
kutokana na kukiuka maadili ya uongozi hawakuweza kufika hata baada ya kupewa
barua za kuitwa na kamati ya maadili hivyo baraza kuu limechukua maamuzi kwa
kufuata katiba yake ya mwaka 1984.
Alisema
kwa mujubu wa tuhuma zilizotolewa na kamati ya maadili ni pamoja na viongozi
hao kupewa maelekezo na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe sambamba na
kula njama ya kukihujumu chama ikiwemo kushiriki operesheni iliyoandaliwa na
Chadema iliyoitwa (Ondoa Msaliti Buguruni), jambo linalokiuka katiba ya CUF.
Amewataja wabunge hao viti maalum na Madiwani waliovuliwa uanachama kuanzia
leo 24/7/2017 ni Riziki Shahali Ngwali, Saverina Mwijage, Salma Mwassa, Saumu
Sakala, Riziki Lulida, Mgeni Jadi kadika, Raisa Abdallah Mussa, Miza Bakari,
Halima Ali Mohammed, Khadija Al Kassim, Leila Hussein Madibi (Diwani viti maalum
ubungo) pamoja na Elizabeth Magwaja (Diwani viti maalum Temeke).
No comments