Breaking News

MHE MPINA: WACHUKULIENI HATUA KALI WANANCHI WATAKAOKAIDI KUTII MAAGIZO YA SERIKALI


Naibu waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe luhanga Mpina akiongoza zoezi la kufanya usafi katika eneo la mchikichini manspaa ya ilalajjni Dar es salam.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina Akisikiliza maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa kampuni ya usafi ya kejenjere trading Bw Mathew Andren ambayo imekuwaikiendesha zoezi la usafi katika manispaa ya ilaa kata ya mchikichini.

Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Luhaga Mpina amewataka viongozi Wilaya ya Ilala kuwachukulia hatua kali watu wanaokaidi kutunza mazingira yanayowazunguka.

kauli hiyo ameitoa jijini Dar es salaam wakati alipokuwa akishiriki katika zoezi la usafi wa kila mwisho wa mwezi.

Amesema kuwa ili kuweza kuhakikisha zoezi hilo linatimia na kuwashirikisha wananchi wote, ni lazima viongozi  wawachukulie hatua kali wananchi ambao wanakaidi kushiriki katika zoezi hilo kwani lipo kwaajili ya  kuiokoa jamii na magonjwa mbalimbali ya mlipuko.

“Ninyi viongozi mnatakiwa kuwachukulia hatua kali wale wananchi wachache wanaokaidi kushiriki katika usafi, kwani haiwezekani watu wailaumu Serikali kwa kila kitu, sisi viongozi wa juu tuleteeni wale walioshindikana ili tuweze kuwashughulikia,”amesema Luhaga.

Aidha, katika hatua nyingine, Luhaga amewataka wananchi kuunga mkono hatua za zinazochuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwani anania ya dhati kuleta maendeleo ya nchi.

Hata hivyo, pamoja na hayo, Mpina ameongeza kuwa katika awamu hii ya TanoTanzania imepata Rais wa kipekee ambaye amekuwa mfano wa kuigwa barani Afrika na duniani kote.


No comments