KAULI YA SPIKA NDUNGAI MARA BAADA YA KUPOKEA BARUA WABUNGE 8 WA CUF KUFUKUZWA UANACHAMA
Spika
wa Bunge, Job Ndugai amesema amepokea barua kutoka kwa Mwenyekiti wa CUF,
Profesa Ibrahim Lipumba ya kuwafukuza uanachama wabunge wanane wa chama hicho.
Katika
taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari leo Jumanne, Julai 25, Spika
amesema suala la kuwaondoa wanachama ni la utashi wa vyama vyenyewe na kila
chama kina utaratibu wake.
“Hivyo
bado naendelea kuitafakari barua hiyo na taarifa rasmi kuhusu maamuzi yangu kwa
wabunge waliofukuzwa nitaitoa hapo baadaye,” amesema.
Wabunge
waliofukuzwa uanachama na Lipumba ni Silvanus Mwijage, Saumu Heri Sakala, Salma
Mwassa, Riziki Shahari Ngwali na Raisa Abdallah Mussa.
Wengine
ni Miza Bakari Haji, Hadija Salum Ally Al-Qassmy na Halima Ali Mohamed, (MB).
Miongoni
mwa makosa yaliyotajwa katika barua ya Lipumba ni pamoja na wabunge hao
kukihujumu chama katika uchaguzi wa marudio wa madiwani wa tarehe 22 Januari,
2017 na kumkashifu na kumdhalilisha Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho,
(Lipumba).
Makosa
mengine ni kumkashifu Naibu Katibu Mkuu na Mbunge wa Kaliua, Magdalena Sakaya,
(MB) pamoja na wakurugenzi wa chama.
No comments