Breaking News

CHAWATA:WALEMAVU WAPEWE NAFASI STAHIKI KATIKA FULSA ZINAZOJITOKEZA NCHINI.

Chama cha walemavu nchini CHAWATA,  kimeiomba serikali inayiongozwa na Rais John Pombe Magufuri kuwapa nafasi stahiki pamoja na kuwapa nafasi katika fulsa zinazojitokeza ili waweze kutumika katika ujenzi wa taifa na maendekeo ya taifa kwa ujumla. 

Mwenyekiti wa chama cha walemavu nchini (CHAWATA) Bw. John Mlabu alisema, jamii ya watu wenye ulemavu wamekuwa wakipata shaka katika mipango wa nchi kuelekea kwenye uchumi wa kati sambamba na sera ya tamzania ya viwanda.

"watu wenye ulemavu tunapata shaka kushiriki katika mipango hii kwani tumekuwa tukiachwa nyuma watu wenye ulemavu kila fuksazinazojitokeza kundi letu linabaki nyuma kwa muda mrefu hususani katika nyanja za kielimu, uchumi, siasa, utamaduni na kijamii" alisema John Mlabu.

Hata hivyo chama hicho kimempongeza Rais John Magufuri kwa hatua ambazo amet=kuwa hakichukua za kuzuia wizi wa asilimali za nchi pamoja na kuiweka nchi katika uchumi wa kati na viwanda, pia kuwajali watu wa kipato cha chini wakiwemo maskini katika taifa hili.

Aidha Bw.Mlabu wamemwomba Rais Magufuli kutokana na usafiri wa bajaji kuwa maalum kwa matumizi ya walemavu wameiomba serikali kuondoa kodi kwa vyombo ivyo pamoja na serikali kutoa kwa mkopo ya Bajaji kwa walemavu kupitia umoja wao wa waendesha Bajaji mkoa wa Dar Es Salaam ambao watazitawanya nchini kwa walengwa ambao ni wanachama wao.

No comments