Breaking News

DC Hapi Amaliza Mgogoro Wa Ardhi Uliodumu Zaidia Ya Miaka 20

Wakazi waishio Kunduchi kata ya Mtongani wametakiwa kuwa na amani kwakuwa serikali imesikia kilio chao hivyo haitowaondoa katika makazi hayo na badala yake watapimiwa maeneo yao rasmi.

Akizungumza jijini Dar es salaam na Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Mhe. Ally Hapi katika mkutano na wakazi wa Kunduchi Mtongani  kuhusu mgogoro wa ardhi uliokuwa ukiwakabili kwa zaidi ya miaka 20 eneo ambalo awali lilikuwa machimbo ya kokoto.

Mhe.Hapi alisema amesikia mapendekezo ya manispaa na halmashauri ya Kinondoni na nmekubaliana nayo hivyo  kuwaeleza wakazi wanaoishi katika eneo hilo kuwa hakuna mtu yeyote atakayekuja kuwaondoa makazi yao katika eneo hilo hivyo wawe na amani.

“Ameiagiza na kuielekeza manispaa ya Kinondoni kuanza upimaji na kuhakikisha hati zinapatikana mapema pamoja na kutenga maeneo muhimupindi wanapopima  kama barabara, hospitali, shule na polisi” alisema Mhe. Hapi.
Aidha Mhe Hapi amemuagiza Katibu tawala kuandika barua chuo kikuu cha Ardhi  ili kuomba wataalam kwenda kanza kufanya kazi ya upimaji katka eneo hilo na kutoa wito watajadili kuona kama kutakuwepo na uwezekano wa wataalam hao kuweza kuendesha zoezi la upimaji bila gharama zozote.
Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. JOHN POMBE MAGUFULI iko makini na yenye kuwajali wananchi wake hivyo suala lolote linalohusu ardhi au kudhulumiwa watoe taarifa kwakuwa serikali ipo tayari kupigania haki za wanyonge.
Kwa upande wake mstahiki meya wa Manispaa ya Kinondoni Mhe.Benjamin  Sitta amempongeza Diwani wa kata kunduch Mhe. Maiko Urio kwa kazi nzuri na hatua ambazo amekuwa akizichukua katika kuwaletea wananchi wa kata hiyo maendeleo hivyo kuwataka wananchi kuwatumia viongozi wao kubainisha changamoto zao hili ziweze kupatiwa ufumbuzi kwani maendeleo yanapatikana kwa kushirikiana na sio kwa itikadi Vyama.
Mapema akimkaribisha stahiki meya wa kinondoni Diwani wa kata ya kunduchi Mhe. Maiko Urio alisema kata hiyo imekuwa na changamoto nyingi lakini kutokana na ushirikiano anaopewa na meya pamoja na mkuu wa wilaya ya kinondoni amekuwa akiweza kutatua chamgamoto mbalimbali za wananchi kwa wakati.(Picha na Moshi Shabani)

No comments