BODI MASJID RIDHWAA KUJENGA CHUO CHA KISLAM NCHINI CHA AINA YAKE.
Bodi
ya wadhamini ya Masjid Ridhwaa (RTMR) Mkwajuni ya Kinondoni jijini Dar es
Salaam kuanza ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kiislam nchini kitakachowezesha wahitimu
kujiajili na kuajiliwa.
Akizungumza
mapema leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Bodi ya hiyo Bw. Alhaj Suleiman
Seif Nassor alisema ujenzi huo wa ghorafa tano ambao unakadiliwa utagharimu
shilingi bilioni 2.
Alisema
ujenzi huo utakapo kamilika chuo hicho utakifanya chuo hicho kikuu waislam Tanzania
(MUTA) kuwa moja ya chuo cha mfano kwa kuzalisha wahitimu ambao watakuwa
wameandaliwa vizuri na kuwa na uwezo wa kujiajili pamoja na kutoa ajira kwa
wengine mara baada ya kuhitimu.
Bw.
Nassor alisema katika kuunga sera ya serikali ya awamu ya tano inayongozwa na
Rais John Pombe Magufuli ya kujenga tanzania ya Viwada vya kati ndio jambo
lilowasukuma kuamua kuanzisha chuo hicho ambacho kutaandaa wasomi ambao pindi
watakapo hitimu masomo yao wataweza kujiajili na sio kungoja kuajiliwa.
“Azma
kubwa ya kuanzishwa chuo hicho ni kuendeleza vijana kitaaluma na kisayansi kwa kuzingatia
sera ya serikali ya awamu ya tano ya kujenga Tanzania ya viwanda vya kati”
Alisema Bw. Nassor.
Tumepania
kutoa mchango kwa kuitikia wito wa Rais Magufuli wa kuanzisha viwanda vya kati kwa kuweka wasomi wenye
mwelekeo wa kidigitali kwa mafunzo na vitendo zaidi ili kuondoa ugonjwa sugu
kwa wahitimu kutafuta kazi.
Aidha
bodi hiyo imetoa pongezi Rais Dkt.John Pombe Magufuri kwa kazi nzuri aliyoifanya
kwa kipindi cha miaka 2 tangu kuingia madarakani kwa hatua anazochukua kuziba
mihanya ya wizi na ubadhilifu wa asilimali za nchi.
"Tumefurahishwa
sana kwa Rais Magufuli kwa namna alivyofanikiwa kuinyoosha nchi, sambamba na kuwaokoa
vijana wengi ambao walikuwa wamejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya”.
Alisema Nassor.
Alisema
Bodi hiyo tayali ameshaiomba serikali ya Rais Magufuli kubaini na kubadili muundo
wa shahada uliopo kwa sasa kwani unawaandaa wahitimu kutafuta ajira serikalini
na kwenye makampuni binafsi badala yake kuandaa masomo yatakayo waandaa
kujiajili tangu wakiwa katika mwaka wa pili wa masomo ya kidigitali.
Pia
alibainisha kuwa (MUTA) imejipanga kuajili walimu wasiopungua 42, sambamba na
kujenga misikiti, vituo vya elimu, vituo vya afya na kufanya miradi ya uchumi
kwa kuzingatia misingi ya kiislam pamoja na kufanya mambo yote ya maendeleo.
No comments