KADA WA CCM KUZINDUA KAMPENI YA “MAGUFULI BAKI” NCHI NZIMA.
Aliyekuwa
Mgombea Ubunge Jimbo la Sengerema kura za maoni CCM 2015,Bw.Laurence Mabawa akifafanua jambo katika mkutano wake
na waandishi wa habari mapema leo jijini dar es salaam, kushoto kwake ni Bi.
Georgina Misana Afisa habari Idara ya Habari malezo
Dar
es salaam
Watanzania
wametakiwa kumwunga mkono jitihada zinazofanywa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa
Tanzania Mhe John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa na nzuri anayoendelea kuifanya
ya kutetea na kupigania rasilimali za taifa.
Wito
huo umetolewa Jijini dar es salaam na aliyekuwa mgombea ubunge wa Jimbo la Sengerema
kura za maoni CCM 2015, Bw. Laurence Mabawa alisema ni vyema watanzania wote
bila kujali jinsia, dini wala makabila kumpongeza na mkumtia moyo Rais na
serikali yake na sio kumkatisha tamaa.
Alisema
pamoja na jitihada zote anazoendelea kuzifanya Rais Magufuli wapo baadhi ya
wanasiasa na kikundi cha watu kimeibuka na kuanza kutoa lugha za mahudhi na
kejeli kuhusu jitahada hizo sambamba na kwa wananchi wanaojitokeza hadharani
kumpongeza rais na serikali yake.
Kundi
hilo limekuwa likiendesha propaganda katika mitandao ya kijamii na kupitia
vyombo vya habari kuwa watu wanaojitokeza hadharani kuwa wanajipendekeza jambo
ambalo si la kweli kwani kwa mujibu wa katiba ya jamhuri ya muunganowa tanzania
ya mwaka 1977 ibara ya 18 inatoa nafasi kwa kila mtanzania kutoa maoni yake.
Aidha
Bw. Mabawa aliongeza kuwa kwa kutambua na kuthamini mchango wa Mhe rais ameamua
kuanzisha kampeni ya “MAGUFULI BAKI’ ambayo itahusisha mikoa yote ya tanzania
bara kwa kuwafikia wanafunzi wa sekondari na wananchi kumwunga mkono Rais
Magufuli kuendelea kusimamia msimamo wake wa kuwatetea watanzania wanyonge na
maskini.
Alisema
kupitia kampeni hiyo ambayo itaendeshwa kupitia mitandao ya kijamii maalum
pamoja na vyombo vya habari itawapa fursa wananchi kutoa maoni yao kuhusu
utendaji wa Rais Magufuli na serikali ya awamu ya tano kwa ujumla ikiwa ni kupongeza
au hata kukosea.
No comments