RAIS MSTAAFU WA NIGERIA MHE. OLUSEGUN OBASANJO AMPA TANO RAIS MAGUFULI
Rais Mstaafu wa Nigeria Mhe. Olusegun
Obasanjo amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John
Pombe Magufuli kwa kuonesha mfano bora katika Bara la Afrika katika kusimamia
uchumi na kutetea maslai ya nchi katika uwekezaji.
Mhe. Rais Mstaafu Obasanjo ametoa
pongezi hizo leo tarehe 20 Juni, 2017 muda mfupi baada ya kukutana na kufanya
mazungumzo na Mhe. Rais Magufuli Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Mhe. Rais Mstaafu Obasanjo amesifu
juhudi za Mhe. Rais Magufuli kuwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka
maeneo mbalimbali duniani na kusimamia ipasavyo sera ya kuhakikisha nchi
inanufaika, badala ya kuacha wawekezaji wakijinufaisha wenyewe na nchi
kuambulia kiasi kidogo cha mapato.
“Nimepita
katika nchi kadhaa zikiwemo Msumbiji, Malawi na sasa nipo hapa Tanzania, na
huko kote nazungumzia masuala ya uchumi na namna nchi zetu za Afrika zinapaswa
kunufaika na uwekezaji katika maeneo mbalimbali.
“Uchumi wa
Tanzania unakwenda vizuri sana, na juhudi za Mhe. Rais Magufuli za kuhakikisha
nchi yake inanufaika na uwekezaji ni suala muhimu sana na la mfano, ameonesha
mfano mzuri kwa viongozi wa Afrika na hii ndio njia pekee itakayotuwezesha
kukuza uchumi wetu, hatuwezi kuendelea kuwaacha wawekezaji wananufaika wao na
sisi kuambulia kiasi kidogo sana” amesema Mhe. Rais
Mstaafu Obasanjo.
No comments