SHEIKH JALALA: VIJANA TUTUMIE DINI ZETU KUDUMISHA AMANI, UMOJA, UTULIVU NA UPENDO ULIOPO NCHINI
Kiongozi
Mkuu wa kiroho wa waislam wa dhehebu la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh Hemed
Jalala akizngumza na wanahabari mara baada ufunguzi wa semina, Katika ukumbi wa
Nkuruma chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM)
Mtoa
mada katika semina hiyo Dr Josephat Muhoza ambaye ni Mtaalamu wa Falsafa Kutoka
Chuo Kikuu cha Dar es salam akizungumza na Wanahabari nje ya ukumbi wa Nkuruma, chuo kikuu cha dar
es salaam.
Washiriki
wa semina hiyo wakitatilia kwa umakini mada zinazowasilishwa
Dar es salaam
Vijana
nchini Tanzania wametakiwa kuendelea kutumia dini zao kama viungo vya kudumisha
Amani, utulivu, na upendo uliopo sasa
nchini badala ya kutumia dini zao kutengeneza migogoro na mifarakano katika
jamii jambo ambalo lina madhara makubwa katika ustawi wa taifa.
Akizungumza
mapema leo jijini Dar es Salaam Kiongozi Mkuu wa kiroho wa waislam wa dhehebu
la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh Hemed Jalala mara baada ya ufunguzi wa
semina maalum iliyofanyika Ukumbi wa
Nkuruma (UDSM) chuo kikuu cha Dar es salaam katika ambayo imewakutanisha
wasomi, wanazuoni na vijana kujadili namna ya kumuunganisha Mwanadamu na dini
yake, sambamba na kutambua Tunu zilizopo katika dini yake.
Alisema
kwa sasa dunia ipo hatarini na inakabiliwa na wimbi la kuweza kuibuka kwa vita vya
wenyewe kwa wenyewe ambavyo katika nchi nyingi dini ndio kimekuwa kichocheo
kikubwa cha migogoro jambo ambalo alisema limepelekea wao kuandaa semina hii
kwa lengo la kuwakutanisha Vijana Pamoja na wataalam mbalimbali kuwakumbusha
namna bora ya kuitumia dini yao kulinda Amani na kuepuka migogoro.
“Tanzania
inasifa ya Amani, upendo, utulivu, kuheshimiana, kutokubaguana, hivyo vijana
tunahitajika kuhakikisha kuwa tunaenzi Tunu hizi kwa hali na mali ili tuendelee
kuwa na sifa ya kisiwa cha Amani duniani”alisema Kiongozi huyo wa Dhehebu la
Shia nchini.
Kwa
upande wake Mwanafalsafa wa kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam Dr Josephat
Muhoza akizumza mara baada ya ukizungumza katika semina hiyo amewataka
watanzania kutanguliza Ubinadamu mbele na kisha dini zao baadae kwani kwa
kufanya hivyo watakuwa wamejiepusha na migogoro kama inayoshuhudiwa katika
mataifa mengineyo duniani.
No comments