Breaking News

RIPOTI YA UMOJA WA WAINJILISHAJI WA KIKRISTO TANZANIA (UWAKITA) RAIS MAGUFULI AMEANZA VIZURI KWA KUZIBA MIANYA YA RUSHWA NA KUSIMAMIA NIZAMU YA KAZI,

Mwenyekiti wa umoja wa wainjilishaji wa kikristo Tanzania (UWAKITA)Samsoni Bullengi akifafanua jambo mbele ya waaandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo mara baada ya kusomwa kwa ripoti ya tathimini ya mwaka mmoja tangu kuingia madarakani kwa serikali ya awamu ya tano,

Frank Wandiba Dar es salaam,

Umoja wa Wainjilisti  wa Kikristo Tanzania (UWAKITA), umetoa ripoti ya mwaka mmoja tangu kuingia madarakani serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe.Rais John Pombe Magufuli.

Akisoma ripoti  hiyo mapema leo  kwa niaba ya Umoja wa wainjilisti wa kikristo mjumbe wa umoja huo bwana Elieza Shonza alisema kwa mujibu wa tathmini ya ripoti inaonyesha kuwa Rais Magufuli ameanza vizuri katika maeneo mbalimbali kama kuziba mianya ya rushwa pamoja na ubadhirifu wa mali za umma nchini.

Alisema ripoti hiyo pia imeonyesha kuwa Rais Magufuli pamoja na hatua mbalimbali za makusudi anazoendelea kuchukua kama nizamu ya kazi, kutetea wanyonge, kukusanya kodi pia amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha  wananchi wa kipato cha chini nao wananufaika na rasilimali zilizopo nchini.

Aidha Bw.Shonza aliongeza kuwa pamoja na hatua nzuri ambazo amekuwa hakichuka mhe magufuli pia ripoti hiyo imebaini kuwepo kwa viashiria vya udini kufatia na baadhi ya viongozi kutoa kauli na matamko ambayo wamekuwa wakitoa hivyo kuzua sintofahamu  jambo ambalo si jema kama likiachwa liendelee.

Akitoa mfano wa kauli ambazo waona zinaweza kusababisha msuguano kwa madhehebu ya imani tofauti kuwa ni kauli aliyoitoa mkuu wa mkoa wa dar es salaam mhe Paul makonda wakati akizindua ujenzi wa jingo litakalokuwa ofisi ya makao makuu ya bakwata nchini ambalo linagharim zaidi ya Bilioni 5.

Alisema Umoja wa wainjilisti tanzania unamwomba mkuu wa mkoa wa dar es salaam kujitokeza na kutolea ufafanuzi juu ya fedha ya ujenzi wa Jengo la makao makuu ya baraza kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), fedha hizo zinatoka katika mfuko gani hili kuondoa dhana potofu iliyopo kwa watanzania,

Bwana Shonza aliongeza kuwa kama serikali inagharamia ujenzi huo ieleze uhalali wake wa kusimamia moja kwa moja ujenzi wa taasisi ya dini hatua ambayo ni kukiuka katiba ya Jamhuri wa Muungano ibara ya 19.


No comments