Breaking News

PICHA: MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA KICHINA 21 JAN 2017 JIJINI DAR

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye mara baada ya kuwasili katika viwanja vya mnazi mmoja kwa ajili ya kufungua sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Jamhuri ya watu wa China leo jijini Dar es Salaam. Katikati ni Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga. (Picha zote na Frank shija & Shamimu Nyaki)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam leo wakati hafla ya kufungua sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa Jamhuri ya watu wa China.China inasherehekea Mwaka Mpya ambapo mwaka huu umepewa jina la Jogoo (Rooster). 
Balozi wa China nchini Tanzania Balozi Dkt. Lu Youqing akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan (wapili kutoka kulia) akiwaongoza viongozi na wananchi wakati wa kuimbwa wimbo wa Taifa katika hafla ya maadhimisho ya waka mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye, Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akimsikiliza kwa makini Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya vikundi mbalimbali vya burudani kupitia Sanaa wakionyesha umahiri wao wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Baadhi ya vikundi mbalimbali vya burudani kupitia Sanaa wakionyesha umahiri wao wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Kijana wa Kichina akitoa burudani ya sarakasi wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Vijana wa Kichina wakitoa burudani ya sarakasi wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Vijana wa Kitanzania wakitoa burudani ya Kung Fu wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 70 na laki nne kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Chato kutoka kwa Balozi wa China nchini Dkt. Lu Youqing wakati wa hafla ya uzinduzi wa sherehe za maadhimisho ya Mwaka Mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 
Ru Ling Mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Soma China consulting And service, walishiriki katika maadhimisho ya mwaka wa kichina 2017 katika viwanja vya mnazi mmoja jijini dar es Salaam kwa kutoa elimu juu ya fursa za kujiunga na vyuo vikuu vilivyopo nchini china kwa watanzania

Baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea katika hafla ya kuadhimisha mwaka mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. 

Baadhi ya washiriki wa maadhimisho hayo wakitembelea baadhi ya mabanda yaliyopo katika viwanja vya Mnazi Mmoja ikiwa ni sehemu ya maadhimisho yam waka mpya wa China leo jijini Dar es Salaam. China wanasherehekea mwaka mpya leo na kesho katika viwanja vya Mnazi Mmoja kuanzia saa 4:00 asubuhi hadi saa 11 jioni. 

No comments