Breaking News

HUDUMA YA UPANDIKIZWAJI WA VIFAA VYA USIKIVU YAANZA RASMI NCHINI.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa huduma ya upandikizwaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto uliofanyika jijini Dar es salaam, kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili Prof. Lawrence Museru. 
 Mkurugenzi wa kampuni inayotoa huduma na kuuza vifaa vya usikivu ya Medel Bw. Mohamed Disouky wa kwanza kushoto akimpa maelezo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya wa pili kulia jinsi huduma hiyo inavyotolewa wakati wa uzinduzi wa huduma ya upandikizwaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto uliofanyika jijini Dar es salaam, wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili Prof. Lawrence Museru.
Baadhi ya wazazi wa watoto wenye matatizo ya usikivu wakiwa katika foleni ya kusubiri huduma ya upandikizwaji wa vifaa vya usikivu wakati wa uzinduzi wa huduma ya upandikizwaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto uliofanyika jijini Dar es salaam. 

Na Ally Daud-MAELEZO
HUDUMA ya upandikizwaji wa vifaa vya usikivu kwa watoto imeanza kutolewa rasmi nchini katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya wataalamu wahuduma hiyo kurejea wakitokea mafunzoni nchini India ili kuweza kusaidia watanzania hususani watoto wenye matatizo ya kusikia.

Akizindua huduma hiyo katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Uisubisya amesema kuwa Huduma hiyo imekua hadimu nchini hivyo kufanya kugharamia kiasi kikubwa cha fedha kwenda kuwatibia nje ya nchi.

“Kwakweli huduma hii ya kupandikiza watoto vifaavya usikivu italeta msaada mkubwa kwa watanzania na kuokoa gharama takribani shilingi milioni 80 kwa kila motto ambaye alitakiwa kwenda kutibiwa nje ya nchi” alisemaDkt. Ulisubisya.

Aidha Dkt.  Ullisubsya amesema kuwa wazazi wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kugundua mapema matatizo ya watoto na kuwaleta katika Hospitali ya Muhimbili ili wapate taratibu za kupata huduma hiyo bila ya kuchelewa na kupata madhara makubwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Muhimbili Prof. Lawrence Museru amesema kuwa Huduma hiyo ambayo ilikua inafuatwa nje ya nchi sasa inafanyika nchini ikiwa ni jitihada za serikali katika kuokoa gharama za matibabu nje ya nchi.

AidhaProf.Museru amesema kuwa hadi kufikia Januari 2017 MNH itaanza kufanya upasuaji na kupandikiza vifaa vya usikivu ikiwa ni huduma iliyokamilika bila ya kwenda nje ya nchi hivyo kupelekea kupunguza gharama zaidi na kusogeza huduma karibu.

“Hapa tulipofikia sio mwisho wa kutoa huduma hii ,tunataka kufikia Januari 2017 tuwe tunafanya upasuaji kabla ya kupandikiza vifaa vya usikivu ikiwa ni huduma kamili na tutakuwa tumefikia baadhi ya malengo tuliyojiwekea mpaka kufikia muda huo” alisema Prof.Museru

AidhaProf.Museru amesema kuwa Serikali ilianza jitihada za kuile tahuduma hii nchini miaka mitatu iliyopita kwa kushirikiana na kampuni ya kuuza vifaa vya kupandikiza vifaa vya usikivu ya Medel kutoka nchini Misri.

Kwa upande wao wazazi wa motto aliyepandikizwa kifaa cha usikivu Angel Ibrahimu (4) mkaziwa Mbeya amesema kuwa anaishukuru Serikali kwa jitihada zake za kufanikisha huduma hiyo kwa mtoto wake kwani lilikua tatizo ambalo asingeliweza kulitatua kwa uwezo wake.

Katika ufunguzi wa huduma hiyo ambayo itakua endelevu nchini imepandikiza vifaa vya usikivu kwa watoto 16 hivyo kuokoa kiasi cha shilingi Mil 300 kama wangeenda nje ya nchi kufata huduma hiyo, fedha hizo zitapelekwa kusaidia katika utoaji wa huduma nyingine

No comments