Breaking News

ASENGA AMEWASHAURI VIONGOZI NA WATENDAJI, KUACHA KUFANYA KAZI ZAO KWA KUWEKA MBELE ITIKADI ZA VYAMA.

Diwani wa kata ya Tabata mhe Patrick john Asenga amewashauri viongozi na watendaji wa mitaa wakiwemo mwenyekiti wa mtaa wa msimbazi mama kuacha kufanya kazi zao kwa kuweka mbele itikadi za vyama pindi wanapotatua kero za wananchi wa eneo hilo na kusisistiza pia ipo haja ya kutambua mipaka ya utendaji kazi zao.

Ushauri ameutoa jijini Dar es Salaam mara baada ya kupokea taarifa kuhusu kusitishwa kwa mkutano wa adhara ambao ulikuwa umepangwa kufanyika katika kata ya msimbazi mama kufatia uongozi wa serikali ya mtaa huo kupeleka taarifa alizodai kuwa ni za kuposhaji kwa mkuu wa mkoa dare s salaam na jeshi la polisi ili kuzuia kufanyika kwa mkutano huo.

Alisema nimepokea taarifa kutoka kwa jeshi la polisi kuwa taarifa za kiintelejensia zinanyesha kuwa kuna uwezekano wa kutokea fujo katika mkutano huo pia kutokana na siku hiyo kuwa jumapili jeshi hilo halina na askari wa kutosha kulinda mkutano huo hivyo kumtaka kusitisha mkutano huo.
Mhe Asenga aliongeza kuwa kwa mujibu wa taarifa alizonazo hatua hiyo ya jeshi la polisi imechukuliwa baada ya viongozi wa mtaa huo kutoa taarifa za upotoshaji kwa jeshi hilo kuwepo kwa viashiria vya uvunjifu wa amani hivyo kulitaka jeshi hilo kutokutoa kibali cha mkutano huo.

Akielezea lengo la kufanya mkutano huo mhe asenga alisema mkutano huo ambao sio wa kiitikadi za kichama kutokana na kutoa mwaliko kwa watendaji mbali mbalia na hata jeshi la polisi alikuwa na lengo la kukutana na wanachi wa kata hiyo kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali za maendeleo wanazokutana nazo ili kuweza kutafutia ufumbuzi.


Aidha mhe Asenga amewataka wananchi wa mtaa huo kuwa na subira kwani amekubali na kutii agizo la polisi kutofanya mkutano siku hiyo, ila ataanza utaratibu mpya wa kuomba kibali kingine cha kufanya mkutano katika eneo hilo hivyo kuwataka kuendelea kuwa na subira mpaka hapo watakapotangaziwa tena tarehe ya mkutano mwingine.

No comments