MAUZO YA HISA YASHUKA KWA ASILIMIA 81
Na Frank wandiba
MAUZO katika
Soko la Hisa Dar es salaam (DSE) yameshuka kwa asilimia 81 kutoka Tsh. Bilioni
9 mpaka kufikia shilingi bilioni 1.7 kutokana na kushuka kwa idadi ya uuzaji wa
hisa kufikia shilingi 340,000 kwa wiki hii.
Akitoa
taarifa ya kila wiki mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es salaam Afisa
Mwandamizi wa masoko wa (DSE) Bi. Mary Kinabo amesema kuwa mauzo hayo yameshuka
kutokana na ukubwa wa mtaji wa soko kushuka kwa asilimia 2.79 kutoka trilioni
21.3 kufikia trilioni 20.7.
Amesema
ukubwa wa mtaji kutoka makampuni ya ndani umebaki kwenye kiwango kile kile cha
shilingi trilioni 8.2 kuma wiki iliyopita.
Aidha Bi.
Mary amesema kuwa licha ya idadi ya mauzo kushuka Benki ya CRDB imeshika nafasi
ya kwanza katika kuuza na kununua hisa kwa asilimia 53 ikifuatiwa na kampuni ya
Bia nchini (TBL) kwa asilimia 35 huku kampuni ya Swissport ikishika nafasi ya
tatu ya kununua hisa kwa asilimia 3.
Pia Bi. Mary ameongeza kuwa licha ya viashiria vya
soko kushuka kwa alama 36.6 kutokana na bei za hisa kutoka TBL kushuka kwa
silimia 1.08, huku viashiria vya huduma za kibenki na kifedha vikipanda
kwa alama 3.64 baada ya mauzo ya DSE kupanda kwa asilimia 11.5.
Share
No comments