Breaking News

WIZARA YAPOKEA MUUNDO UNAOPENDEKEZWA WA SHIRIKA LA POLISI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni akizungumza wakati wa majadiliano kati ya timu ya wizara na wataalamu wa Muundo Unaopendekezwa wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi ambapo wataalamu waliwasilisha muundo huo mbele ya wizara. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara, Ally Senga Gugu. Kikao hicho kimefanyika Makao Makuu ya wizara jijini Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ally Senga Gugu akizungumza wakati wa majadiliano kati ya timu ya wizara na wataalamu wa Muundo Unaopendekezwa wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi ambapo wataalamu waliwasilisha muundo huo mbele ya wizara. Kushoto ni Waziri wa wizara hiyo, Mhandisi Hamad Masauni Kikao hicho kimefanyika Makao Makuu ya wizara jijini Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Maduhu Kazi akizungumza wakati wa majadiliano kati ya timu ya wizara na wataalamu wa Muundo Unaopendekezwa wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi ambapo wataalamu waliwasilisha muundo huo mbele ya wizara.Kikao hicho kimefanyika Makao Makuu ya wizara jijini Dodoma. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mtaalamu elekezi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Profesa John Kafuku akiwasilisha Muundo Unaopendekezwa wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi mbele ya uongozi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(hayupo pichani).Kikao hicho kimefanyika Makao Makuu ya wizara jijini Dodoma.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imepokea Muundo Unaopendekezwa wa Shirika la Uzalishaji Mali wa Jeshi la Polisi kutoka kwa timu ya Wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakiongozwa na Profesa John Kafuku ambapo Shirika hilo la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi lilianzishwa Machi,29,2013 kupitia Agizo la Rais namba 66 la kuboresha miundombinu na kujenga uwezo wa kiuchumi wa Jeshi la Polisi baada yay a Serikali kupitisha Mkakati wa Maboresho wa Jeshi la Polisi wa miaka mitano unaolenga kujenga usasa,ushirikiano wa jamii na utaalamu.

Akizungumza wakati wa wasilisho hilo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Mhandisi Hamad Masauni alisema adhma ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt Samia Suluhu Hassan ni kuona vyombo vya ulinzi na Usalama vikibakia katika majukumu yake ya msingi ambayo ni ulinzi wa raia na mali zao huku mashirika ya uzalishaji mali yaliyopo katika vyombo hivyo yakiachwa yafanywe shughuli za uzalishaji mali ikiwemo kilimo,uzalishaji wa fenicha,ushonaji wa nguo,utengenezajai wa viatu.

‘Maelekezo ya Mheshimiwa Rais yalikua yapo wazi na yalilenga kuyafanya majeshi yetu yawe na mashirika ambayo yako katika ushindani katika sekta husika ikiwa ya kilimo au viwanda na akataka mapato yanayotokana na mashirika hayo yatumike kuimarisha vyombo hivyo vya ulinzi na usalama’.alisema Waziri Masauni.

Pia amewapongeza wataalamu hao kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa wasilisho la muundo pendekezi huku akiwaomba kujumuisha na maoni yaliyotolewa na wajumbe wa kikao hicho huku akiwaomba kuhakikisha wanarejesha muundo huo wa mwisho ili shirika liweze kuingia kwenye utendaji wa miradi mbalimbali iliyopo mbele yake ikiwemo mradi wa miji salama.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa wizara hiyo,Ally Senga Gugu,Naibu Katibu Katibu Mkuu,Dkt. Maduhu Kazi,Kaimu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,Kamishna wa Polisi,Liberati Sabas na Wakurugenzi wa Idara zilizopo chini ya wizara hiyo.