Breaking News

Taasisi Ya Elimu Ya Watu Wazima Yaendelea Kukuza Kwa Elimu Nchini

Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha (kulia) akisisitiza jambo  kwa  Naibu Mkurugenzi   wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima  (TEWW) Taaluma Utafiti na Ushauri Dkt. Kassimu Nihuka wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.Katikati ni Naibu Mkurugenzi   wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima  (TEWW) Taaluma Utafiti na Ushauri Dkt. Kassimu Nihuka,kushoto ni Mhadhiri wa Taasisi hiyo Dkt. Bernadeta Kapinga.
Naibu Mkurugenzi   wa Taasisi ya Elimu ya watu Wazima  (TEWW) Taaluma Utafiti na Ushauri Dkt. Kassimu  Nihuka (katikati) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha (wakwanza kulia) kuhusu utendaji wa Taasisi hiyo ambapo imepata mafanikio kwa kuongeza udahili kutoka wanafunzi 627 mwaka 2009/2010  hadi kufikia wanafunzi 3606 mwaka 2017/2018 kwa ngazi za Astashahada, Stasgahada na Shahada, sawa na asilimia 575kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania bara na Visiwani.
Naibu Mkurugenzi   wa Taasisi ya Elimu ya watu Wazima  (TEWW) Taaluma Utafiti na Ushauri Dkt. Kassimu  Nihuka (katikati) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha kuhusu maktaba ya Taasisi hiyo wakati wa  ziara yake katika Taasisi hiyo mapema leo.
Baadhi ya Watumishi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha (Hayupo pichani) wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha akisisitiza jambo kwa  kwa Viongozi wa Taasisi hiyo baada ya kupewa maelezo kuhusu utekelezaji wa programu ya elimu masafa inayotolewa na Taasisi hiyo mapema leo wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo. Picha na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW).

Na Samwel Gasuku- TEWW
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) imetajwa kutoa mchango mkubwa katika kukuza kiwango cha elimu hapa nchini kwa kuwa umuhimu wake unaonekana katika jamii kupitia wataalamu wanaozalishwa na taasisi hiyo tangu kuanzishwa kwake.

Akizungumza wakati wa ziara yake katika Taasisi hiyo Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. William Tate Ole Nasha amesema kuwa Taasisi hiyo ni nguzo muhimu katika kuchochea ukuaji wa sekta hiyo kwa kuzingatia kuwa inaendana na mahitaji ya sasa.

“Kwa sasa ni muda muafaka wa kuifanya Taasisi hii iweze kuwa mdhibiti mkuu wa elimu ya watu wazima ikiwezekana hata tufanye maboresho ya sheria  iliyoinzisha TEWW ili kuipa nguvu ya kuwa mamlaka” Alisisitiza Waziri Ole Nasha

Akifafafanua Waziri Ole Nasha amesema kuwa ni wakati muafaka kwa Taasisi hiyo kushirikiana na Taasisi mbalimbali katika kuimarisha utendaji  na kuongeza ubunifu ili kuwa na tija zaidi.

Aliongeza kuwa mfumo wa elimu ya Watu Wazima ni wa Kidunia hivyo ni vyema kwa hapa nchini ukaendelezwa ili kuwapa fursa wale waliokosa katika mfumo rasmi kujiendeleza na kutoa mchango wao katika kuleta maendeleo na kukuza uchumi.

Pia alipongeza Taasisi hiyo kwa kufanya kazi kwa bidii na maarifa hali inayomsukuma kuzifanyia kazi changamoto zinazoikabili Taasisi hiyo ili kupanua zaidi wigo wa kutoa elimu yenye ubora unaoendana na mahitaji.

Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi  wa TEWW Taaluma Utafiti na Ushauri  Dkt.  Nihuka  amesema kuwa tangu Taasisi hiyo ilipopata ithibati imefanikiwa kuongeza udahili kutoka wanafunzi 627 mwaka 2009/2010  hadi kufikia wanafunzi 3606 mwaka 2017/2018 kwa ngazi za Astashahada, Stashahada na Shahada, sawa na asilimia 575 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania bara na Visiwani.

”Taasisi yetu kwa kushirikiana na SIDO pamoja na Kiwohede kwa ufadhili wa “ Commonwealth of Learning” imeanzisha programu ya kuzuia ndoa za utotoni kwa wasichana wenye umri kati ya miaka 10-25 katika Mikoa ya Rukwa,Dodoma na Lindi ambapo wasichana 3000 na wanajamii 10,000.” Alisisitiza

Akifafanua amesema juhudi za Serikali zimeiwezesha TEWW kununua vifaa kwa ajili ya Kampasi ya WAMO morogoro na kukarabati kiwanda na ununuzi wa mitambo mipya ya uchapaji itakayochochea na kuongeza tija katika Taasisi hiyo.

Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) ilianzishwa chini ya Sheria ya Bunge Na.12 ya mwaka 1975 na kupewa majukumu mbalimbali ikiwemo kutoa Elimu ya Watu Wazima  kwa wataalamu,wawezeshaji na wasimamizi wa elimu ya Watu Wazima nchini pamoja na kutoa mafunzo ya elimu ya kujiendeleza ngazi ya sekondari nje ya mfumo rasmi kwa njia ujifunzaji huria masafa kwa vijana na watu Wazima waliokosa elimu kwa sababu mbalimbali.

No comments