Breaking News

Benki Ya Pta Yabadili Jina, Sasa Kuitwa Benki Ya Tdb


Mkurugenzi wa Maswala ya Ndani na Uhusiano wa Wawekezaji wa benki ya TDB, Mary Kamari akizungumza kuhusu PTA kubadili jina kuwa TDB na akielezea mipango mbalimbali ambayo benki hiyo wanayo ili kuliwezesha baa la Afrika kupata maendeleo makubwa.
Benki ya biashara na maendeleo mashariki na kusini mwa afrika maarufu kama TPA imebadili rasmi jina la biashara Leo na kuanza kutumia jina la TDB.

Akizungumza mapema leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Maswala ya Ndani na Uhusiano wa Wawekezaji wa benki ya TDB, Mary Kamari alisema kubadili jina kumekuja baada ya miaka kadhaa ambapo ubora wa mali uliongezeka, upatikanaji wa faida, umepanda na ubunifu unatumika ipasavyo, vitu vilivyotokana na mageuzi kadhaa ya muundo mzima wa benki yanayolenga kuimarisha na kuifanya iwe ya kisasa zaidi.
“Tumeongeza kwa kaisi kikubwa uwezi wetu wa kutosheleza mahitaji ya bidhaa na huduma zatu, kupitia mtandao imara tuliojenga ukijumuisha waliowekeza kwetu na wafadhili wetu.
Wanahisa wetu wameongezeka kwa zaidi ya asilimia 50 katika miaka ya karibuni zikiwemo taasisi kadhaa mpya za uwekezaji na nchi wanachama,” alisema Kimari.

Alisema benki hiyo imejipanga kuendeleza utekelezaji wa miradi iliyopo kwenye sekta zenye kupewa kipaumbele kama vile miundombinu, viwanda na biashara ya kilimo katika nchi 21 ambazo inafanya shughuli zake kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
“Usanifu wa jina letu unaashiria kuibuka kwa nguvu mpya na dhamira mpya katika kuimarisha biashara, Maendeleo ya uchumi pamoja na ushirikiano wa kikanda katika kuakikisha kwa dhati kusukuma mbele mageuzi ya kiuchumi na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi” alisema Kimari.


Katika miradi ya karibuni tumechochea kasi yetu na kutoa mikopo katika biashara, ujasiriamali na miundombinu na kuongeza mara tatu kwa fungu letu zima la mikopo katika miaka mitano iliyopita. Tumechangia kwa kaisi kikubwa katika ukuaji wa sasa wa uchumi na maendeleo ya miundombinu katika ukanda mzima.


Alisema benki hiyo imetoa mikopo ili kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na mradi 711 wa Kawe, Dar unaoendeshwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Fibre Optic Backbone Project wa nchini Burunndi, miradi ya nishati endelevu ambayo inafanyika Kenya na Uganda na miradi ya viwanda vya simenti na chuma katika nchi ya Congo DRC, Djibouti, Zambia, Rwanda, Ethiopia na Zimbabwe.

No comments