Breaking News

Washindi 10 wa Shindano La Vipaji Vya Sauti Wapatikana Sasa Kwenda China.

Washindi wa Shindano linalodhaminiwa na kampuni ya Star Media (T) Ltd kupitia StarTimes na chaneli yake ya Star Swahili lilifikia mwisho huku washindi 10 wakiibuka kidedea katika mchakatio wa kuwasaka machampioni hao.

Miongoni mwa watu walioibuka washindi ni Msanii wa filamu Bongo, Koletha Raymond, aliyeibuka mshindi namba moja baada ya kuwabwaga washiriki zaidi ya 25, aliyokuwa akichuana nao kwa ajili ya kuwania nafasi ya kwenda kufanya kazi makao makuu ya Kampuni ya Star Times, nchini China kuigiza sauti ya filamu mbalimbali zilizochezwa kwa lugha mbalimbali.

Shindano hilo lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa LAPF lililopo Millenium Tower Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ambapo washindi 10, wataungana na Koleta kwenda nchini humo kwa ajili ya kufanya kazi hiyo ambayo wataifanya kwa mkataba wa mwaka mmoja.

Washindi hao wamepatikana katika ushindani mkali mbele ya majaji watatu wakiongozwa na wasanii Jacob Steven ‘JB’ na Mrisho Mpoto ‘Mjomba’ ambapo haikuwa kazi rahisi kwa majaji hao na washiriki wenyewe kutokana na ushindani mkali uliojitokeza.

Washiriki 25, watano kutoka Mwanza, watano kutoka Zanzibar na 15 wa Dar es Salaam, walichuana vikali kupata washindi 10 wanaokwenda kufanya kazi hiyo nchini China.

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili kwa mwaka 2017.
Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif akizungumza na waandishi wa habari wakati wa  shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili mwaka 2017 lililofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
Washindi 10 wa shindano la vipaji vya sauti walioshinda kwenda nchini China kufanya kazi makao makuu ya Kampuni ya Startimes  kwenye fainali hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa washindi walioingia kumi bora akipokea zawadi ya simu ya Startimes kutoka kwa Makamu wa Rais wa Startimes Tanzania, Zuhura Hanif mara baada ya kumalizika kwa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili lililofanyika katika ukumbi wa LAPF jijini Dar es Salaam
Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA), Dkt. Seleman Sewangi(kulia) akimkabidhi zawadi ya Television ya Startimes mshindi wa kwanza wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili, Coletha Raymond mara baada ya kuibuka mshindi wa shindano hilo
Mshindi wa kwanza hadi wa tatu wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili mwaka 2017 wakiwa kwenye picha ya Pamoja.
Mshindi wa kwanza hadi wa tatu wa shindano la vipaji vya sauti msimu wa pili mwaka 2017 wakiwa kwenye picha ya Pamoja.

No comments