DIWANI WA VIKINDU MHE NICHOLUS JOHN WAASA WANAFUNZI CHUO CHA WALIMU VIKINDU KUWA MAADILI KIPINDI CHOTE CHA MASOMO
Diwani Wa Kata Hiyo Ya Vikindu Mhe Nicholus John .
Na Sala Mlawas-Dar
WITO umetolewa kwa wanafunzi ambao ni
walimu watarajiwa kuwa na hekima pamoja na busara kwani wanapotoka vyuoni
wanatarajiwa kwenda kuelimisha jamii na sio kupotosha .
Akizungumza na
waandishi Wa habari Jijini Dar Es Salaam Mwenyekiti Wa Bodi Ya Chuo Cha Ualimu
Cha Vikindu Na Pia Ni Diwani Wa Kata Hiyo Ya Vikindu Mhe Nicholus John alisema
ameamua kuwahamasisha wanafunzi Wa chuo hicho kuwa na maadili yanayostaili kwani
wao wasipokua na maadili mazuri ni sawa na kwenda kupotosha jamii wanapotoka
vyuoni.
“ Kitu ambacho kimenisukuma kutoa wito huu ni kufatia kuwepo kwa taarifa kuwa baadhi ya wanafunzi wanaotakiwa kufukuzwa chuo kutokana na kutokuwa na maadili mema ikiwemo vitendo vya utovu wa nizamu na uongo walivyokuwa wanafanya kwa walimu wao” Alisema John.
Diwani Wa Kata Hiyo Ya Vikindu Mhe Nicholus John akifafanua
jambo katika mkutano wake na waandishi wa habari (hawapo pichani)
Mhe john ametaja majina ya wanafunzi hao kuwa ni Husna Hemedi, na Zaituni Omary ambao walikua wamekidhiri kwa utovu wa nizamu na
walimu kuchukua jukumu lakutaka kuwafukuza chuo.
Hata hivyo mhe John alisema ameamua kuwaombea msamaha ili wasiweze kufukuzwa kwani bado miezi
mitatu waweze kufuzu masomo hayo na kwenda kutafuta ajira na pia aliona
atawaumiza wazazi na walezi wao kwani wanafunzi wamekua wakilipiwa ada kwa
wakati na wazazi wakiwa na imani wanawasaidia watoto wao waje
kujiendeleza katika maisha yao .
Aidha Mhe john
aliongeza kuwa chuo hicho kimekuwa na changamoto mbalimbali zinazokikabili pamoja
na ukosefu wa fensi , ukosefu wa ofisi za wakufunzi, ukosefu wa uwanja kwa
ajili ya mazoezi kwa vijana hao.
Pia Mhe John
ameiomba serikali itenge fungu ambalo litaweza kutatatua
changamoto hizo ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu kwani wanatokea maeneo ya
mbali inawadhalimu kuchelewa mda wa vipindi kwa ugumu wa usafiri.
No comments