Breaking News

Naibu Waziri Wa Afya Mhe Ndugulile Azindua Kampeni Ya Upimaji Macho, Shinikizo La Damu Na Kisukari Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani.

Naibu Waziri Wa Afya Mheshimiwa Faustine Ndugulile (Mb) leo amemuwakilisha Makamu Wa Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu katika uzinduzi wa Kampeni Ya Upimaji Macho, Shinikizo La Damu Na Kisukari Mkoani Pwani katika Wilayani Mkuranga.

Katika hatua hiyo Naibu Waziri Amempongeza Mwenyekiti Wa Lions Club kwa jitihada anazofanya za kuunga mkono juhudi za Serikali Ya Awamu Ya Tano kwa kampeni anayoendelea nayo ya  huduma ya upimaji wa afya bure katika jamii.

Aidha, Naibu Waziri Wa Afya ameeleza utafiti uliofanywa na Wizara Ya Afya, Maendeleo Ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Shirika La Afya Duniani (WHO)  na Taasisi Ya NIMR  wa Mwaka 2013, unaohusu Viashiria  Vya  Magonjwa Yasiyo Ya Kuambukiza, umeonyesha Kuongezeka  kwa viashiria hivyo, idadi ya Watanzania wenye shinikizo la damu ni asilimia 25.9% na wagonjwa wa kisukari ni asilimia 9.1%.

"Hii Haikubaliki, ni lazima tuongeze  bidii katika kuyashughulikia magonjwa haya. Ni lazima Kwa pamoja Serikali Na Sekta Binafsi tufanye kazi  kwa bidii katika kupambana na janga hili ambalo visababishi vyake vikubwa ni pamoja na ulaji usiofaa, kutokufanya mazoezi, matumizi ya pombe na tumbaku kupita kiasi " alisema Dkt Ndugulile.

Mheshimiwa Naibu Waziri amesema Serikali inafanya kazi kwa kushirikiana na Wadau katika kutoa elimu kwa jamii kuhusu namna bora ya kujikinga na maradhi yasiyo ya kuambukiza kupitia njia mbalimbali.

Katika hatua hiyo kliniki zipatazo 187 za magonjwa yasiyo ya kuambukiza zimeanzishwa  na kuimarishwa, kuanzia ngazi Ya Vituo Vya Afya mpaka Hospitali Ya Taifa.

Aidha, Mheshimiwa Naibu Waziri alipata fursa ya kutembea kiwanda cha KNAUF ambacho kinajishughulisha na uzalishaji wa Gypsum Board Na Gypsum Plaster Na kuwapongeza kwa juhudi wanazofanya za kuunga mkono Sera Ya Viwanda Nchini


Naibu  Waziri aliwashukuru Uongozi mzima wa Lions Club Dar Es Salaam kwa kushirikiana na Madaktari wa hospitali ya Regency na Wilaya ya Mkuranga kwa kumualika na kuahidi Serikali Ya Awamu Ya Tano itaendelea kuunga mkono juhudi zote wanazofanya na kuahidi kuwapa ushirikiano wa karibu pindi watapohitaji.

No comments