Breaking News

Mhe Zitto Awataka Wachunguzi Wa Kimataifa Kuja Tanzania.

Chama cha ACT Wazalendo kimeiomba Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Benki ya Dunia (WB) kufanya uchunguzi maalumu wa takwimu za kasi ya ukuaji wa uchumi ya robo ya pili ya mwaka na kuchukua hatua endapo itabainika kile anachodai kuwa Serikali ilipika takwimu.
Akuzungumza mapema leo jijini dare s salaam kiongozi wa Act wazalendo Mhe Zitto Kabwe alisema chama hicho kimebaini kuwepo sintofahamu juu ya takwimu zilizotolewa na Serikali za mwezi Aprili hadi Juni mwaka huu kuwepo na mashaka juu ya Usahihi.
Alisema takwimu za Serikali zinaonyesha kasi ya ukuaji wa uchumi katika robo ya pili ya mwaka ni asilimia 5.7, tofauti na za ukokotozi kwa kanuni za kiuchumi anazodai zinaonyesha ni asilimia 0.1.
“Hatujatafuta takwimu nyingine, hizi ni taarifa zilezile zilizotolewa na BoT na NBS lakini ukikokotoa utaona uchumi tulionao unasinyaa badala ya kukua na hali ikiendelea hivi hadi Juni 2018 kutakuwa hakuna uchumi Tanzania,” Alisema Mhe Zitto.
Alisema sababu hiyo inachangia maisha ya Watanzania kuendelea kuwa magumu ilhali Serikali imekuwa ikitoa taarifa za uchumi kukua.
Aidha mhe Zitto amegusia pia takwimu za mapato yanayokusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) akidai nazo haziko sahihi.
Amesema ni vyema wakati TRA ikitoa takwimu zake ikaeleza mapato kwa kila idara bila kuchanganya marejesho na madeni ambayo hayajalipwa.
“Taarifa yao ieleze kinagaubaga mapato ya idara ya forodha, walipa kodi wakubwa na walipa kodi za ndani. Wasiishie hapo, kati ya fedha wanazotaja kukusanya iwekwe wazi madeni na marejesho ni yapi tofauti na inavyofanywa sasa,” amesema.
Zitto ametaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi wa mapato ya Serikali ya Julai na Agosti na kuweka wazi taarifa hiyo.


No comments