Breaking News

LHRC Yaitaka Serikali Kufuta Sheria Ya Adhabu Ya Kifo

Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na waandishi wa habari juu ya kupinga adhabu ya kifo leo jijini Dar es Salaam.

KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeitaka serikali kubadilisha sharia, kuondoa adhabu ya kifo kwa kuweka adhabu mbadala kwenye makosa ya jinai na wafungwa waliopo katika vifungo vya muda mrefu gerezani.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Anna Henga akizungumza na Mtandao wa Matukio360, amesema  kuwa kituo hicho kinaungana na Mtandao wa Kupinga Adhabu ya Kifo Duniani katika maadhimisho ya 15 siku ya kupinga adhabu ya kifo.

Henga amesema adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili ambayo inakinzana na misingi ya utu na haki za binadamu kama ilivyoainishwa katika mikataba mbalimbali ya kimataifa.

“Adhabu ya kifo ni adhabu ya kikatili isiyo ya staha, inayotweza utu wa binadamu, inafanya serikali ionekane pia kama mhalifu kwa kuua, tuitake serikali ibadilishe sharia na kuondoa adhabu ya kifo na kuweka adhabu mbadala kwenye makosa ya jinai na kwa wafungwa waliopo mfano vifungo vya mrefu,” amesema Henga.

Aidha LHRC kime mpongeza Rais John Magufuli kwa kuweka wazi msimamo wake wa kutounga mkono adhabu ya kifo kwani ni ya kinyama na isiyostahili binadamu yeyote.

Kwa upande mwingine Henga ametoa sababu  za kituo hicho kupinga adhabu hiyo. Miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na adhabu kuwa ya kibaguzi kwani mara nyingi wanaopatikana na hatia na kupewa adhabu hiyo ni maskini wasioweza kuwa na ushauri wa kisheria na watu wengine.

Nyingine ni vigumu kuthibitisha kuwa inatekelezwa tu kwa watu ambao wametenda na kukutwa na hatia ya kosa hili au wabaya Zaidi, Adhabu hiyo ikitolewa kwa mtu asiye na hatia kimakosa huwezi kuirekebisha kwani mfumo wa utoaji haki huwa pia na uwezekano wa kuwa na mianya ya makosa.

Ameongeza nyingine kuwa ni adhabu kutompa nafasi mtuhumiwa kujirekebisha bali ni ya kulipiza kisasi na wala haimsaidii mtu yeyote hata familia ya muathirika, hakuna ushahidi wowote kuwa adhabu hiyo inazuia watu wengine kutokwenda makosa kama hayo.

Pia amesema sharia hiyo inamianya ya makosa na ni vigumu kuwa na uhakika kuwa haki itatendeka kila wakati. Wapelelezi –ubambikiwaji wa kesi, changamoto za kiupelelezi, waendesha mashtaka, huweza kufanya makosa, majaji kufungwa mikono kulingana na uwakilishi mbele yao na kubanwa na sharia inayowataka kutoa adhabu ya kifo kwenye makosa tajwa.

No comments