Breaking News

Kauli Ya Mhe Sumaye Kufatia Kunyang’anywa Mashamba Yake

Image result for sumaye
Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye  ametoa ufafanuzi kuhusu Rais Magufuli kuchukua mashamba ya familia yake yaliyopo Dar es salaam na Morogoro.

Akizungumza jijini Dar es salaam leo Sumaye amesema chanzo cha migogoro hiyo ilianza mara baada ya kuondoka ccm na kujiunga na upinzani ambapo tetesi zilivuma kuwa dawa ni kunyang'anywa mashamba.

Sumaye amesema shamba la Mabwepande   lenye ukubwa wa heka 33  ambalo lilimilikiwa kihalali na mtoto wake Frank Sumaye na lingine la mkewe Esta Sumaye lililopo Mvomero lenye ukubwa wa heka 326 yamechukuliwa kwa visasi vya kisiasa.

Aidha amesema walifungua kesi tatu ambapo mahakama ilitoa amri ya serikali kutoingilia mashamba hayo lakini jambo hilo likapuuzwa.

Amehoji kuhusu agizo lililotolewa na Waziri wa ardhi Lukuvi la kuendeleza shamba ndani ya siku 90 huko Mabwepande  eneo ambalo tayari lilishakaliwa na wavamizi ambao serikali iliwalinda kupitia kauli ya mkuu wa wilaya ALLY HAPI kuwa wakae tu.

Amesema shamba la Mvomero tayari liliendelelezwa na kwamba kuna visima viwili,umeme na mifugo na kutoa nukuu ya jibu iliyowahi kutolewa bungeni kupitia wizara ya Ardhi kuwa shamba hilo linatumika kihalali.


Sumaye amesema ni vema  muhimili wa utawala kuacha kuingilia muhimili wa bunge jambo ambalo hivi sasa polisi wamekuwa wakiingia hadi bungeni na kusema haki ya mabavu siyo msingi wa demokrasia.

No comments